KICHAKA CHA SIMULIZI
BLOG YA SIMULIZI ZA GIFT KIPAPA PAMOJA NA TAFSIRI ZA FILAMU KALI
Thursday, June 29, 2017
Friday, August 19, 2016
Saturday, July 9, 2016
WHEN I SAY I LOVE YOU BOOK 1
BY D.G.LWASYE 'GIFT KIPAPA'
Mwanzoni mwa mwaka 2000, mwaka
ambao haukuwa mpya peke yake bali pia ulikuwa ni mwanzo wa karne mpya ya
ishirini na moja. Watu walikuwa wana tarajia mambo mengi sana mwaka huo ikiwa
pamoja na vitisho kama vile mwisho wa dunia na kutokufanya kazi kwa kompyuta,
yote hayo yalikuwa ni chachu zilizoufanya mwaka huo uwe wa kipekee.
Katika ofisi ya makao makuu ya dayosisi ya mbeya
iliyo chini ya dhehebu la kirutheli, kulikuwa na vijana wengi wa rika moja
waliokuwa wamekaa katika mapokezi ya ofisi hiyo iliyopo katika wiliya ya
tukuyu.
Vijana hao walikuwa ni wanafunzi wapya wa shule ya sekondari iitwayo
‘MANOW JUNIOR SEMINARY’
inayomilikiwa na dayosisi hiyo.
Walikuwa hapo wakisubiri basi la shule liwapeleke
mahali ilipo shule yao ili wakaanze masomo yao ya sekondari kwa mara ya kwanza.
Japo wengi wao walikuwa hawafahamiani lakini
wakajikuta wanazoeana katika kipindi hicho kifupi walichokuwa hapo. Waliongea
na kucheka pamoja kwa ujumla wote walikuwa na furaha ya kwenda kujiunga na
masomo ya sekondari hasa hasa sekondari ya bweni, kwani kwao yalikuwa ni maisha
mapya waliokuwa wakiyaota pindi
walipokuwa shule ya msingi, wakiamini kwamba wakiwa bweni watakuwa huru na sheria na miiko ya wazazi
wao.
Waliongea mambo mengi lakini zaidi ni juu ya maisha
ya bweni , kila mmoja aliongea kile alichowahi kusikia kuhusu bweni.
Wengine walisema
wanafunzi wa vidato vya juu wanawatesa na kuwatumikisha wanafunzi wa
kidato cha kwanza huku wengine wakisema hayo yalikuwa ni mambo ya kizamani ,
siku hizi hakuna anyeingilia uhuru wa mwenzake.
“piiii!, piiii!”
Ilisikika honi toka kwenye gari moja la kifahari
aina ya hammer lililokuwa likiingiia katika maegesho ya ofisi hiyo.
Wanafunzi watatu wa kike ndio waliokuwa wakipigiwa
honi hiyo. Walikuwa wamesimama katika maegesho hayo wakipiga stori mpaka
kujisahau. Walisogea pembeni huku wakicheka, waliliangalia gari hilo lililokuwa
na vioo vyeusi yenye uwezo wa kumzuia mtu wa nje asione ndani ya gari.
Matairi ya gari hilo yalisimama mara baada ya
kuegeshwa vizuri katika maegesho hayo kisha mlango wa upande wa dereva
ulifunguliwa na kisha mtu aliyekuwa akiendesha alishuka.
Sura za wale mabinti waliokuwa wakilikodolea gari
hilo zilibadilika ghafla na kujawa na taharuki hata kicheko chao kilikatika,
hakuna yoyote kati yao aliyeamini kile alichokiona.
Hii ilikuwa ni kwa mara ya kwanza kwao kumuona
mvulana wa rika lao akiendesha gari la kifahari namna hiyo, na haikuwa juu ya
gari peke yake bali pia mavazi yake, cheni
pamoja na saa ya mkononi, kila kitu kilikuwa ni ghari ni kama vile walimuona
nyota wa muziki hip hop nchini marekani.
Sekunde chache baada ya kijana
huyo kushuka mlango wa upande wa pili ulifunguliwa ambapo alishuka mzee mmoja
wa makamo alievalia suti ya rangi ya kahawia. mara baada ya kushuka toka ndani
ya gari hilo, mzee huyo aliliangalia jengo la ofisi hiyo kisha akatabasamu,
akaanza kupiga hatua kuelekea ulipo mlango wa ofisi hiyo ambapo yule kijana
aliyekuwa nae alimfuata.
Wale wasichana watatu waliendelea
kumkodolea macho kijana huyo mpaka alipotokomea ndani ya ofisi hizo.
“Mambo ya vibopa hayo!”
aliongea mmoja kati ya wasichana hao akimaanisha mambo ya
matajiri, wenzake hawakuongea jambo lolote zaidi ya kucheka na baada ya muda
mfupi waliendelea na maongezi yao waliyokuwa wakiongea mawanzoni na kusahau
habari za yule kijana, waliendelea kuongea huku wakicheka na kufurahi.
“Unaona basi nikamwambia huwezi kuju…………”,
msichana huyo alikatiza kile alichokuwa akiwaeleza
wenzake na kisha ukimya ulitawala kati yao kwa muda fulani huku wote watatu
wakiwa makini na kitu fulani, hii iliwatokea mara baada ya kijana yule aliepita
wakati ule, akitoka ndani ya ofisi na kutembea kwa mwendo wa taratibu kuelekea
kule alikoegesha gari yao, ukimya uliendelea kuwapo kati ya wasichana hao huku
macho yao yakimnyemelea kijana huyo.
Kijana huyo ambaye kwa muonekano
hakuwa na sura yenye mvuto wala macho yenye kuvutia sana wasichana, yeye
alikuwa wa kawaida sana kiasi cha kuweza hata kudharaulika hata mbele za
msichana yeyote yule mwenye kuumbika, kifupi mvulana huyo alikuwa mbaya wa sura na
hata umbo, lakini cha ajabu wasichana hao walionekana kumkodolea macho kupita
kiasi mpaka kufikia hatua ya kusitisha maongezi yao.
Mvulana huyo alienda moja kwa moja lilipo gari lao
na kuliegamia na kisha kutoa simu iliyokuwepo mfukoni mwake na kupiga namba
fulani. Wasichana wale watatu waliacha midomo wazi kwa mshangao baada ya kuiona
simu ya mvulana huyo ambayo ilikuwa ni simu ya gharama sana kiasi cha wasichana
hao kutowahi kuiona maishani mwao.
“Vipi sister” alianza kuongea
kijana huyo mara baada ya simu aliyokuwa akipiga kupokelewa.
“Tumefika salama tu, ila uchovu
tu” aliendelea kuongea kijana huyo huku bado wale wasichana wakiendelea
kumwangalia,
“Robert Jackson!” aliita mama
mmoja aliyekuwa amesimama kwenye mlango wa kuingilia kwenye ofisi hiyo, kauli
hiyo ilimfanya kijana yule akate simu hata bila ya kuagana vizuri na aliyekuwa
akiongea nae.
“Naam” kijana yule aliitika akiwa
amesimama wima.
“Unahitajika kwenye ofisi ya
Askofu” aliongea mama huyo mara tu akageuka na kuingia ndani ya ofisi hiyo.
“Kumbe anaitwa Robert Jackson”
aliongea mmoja kati ya wale wasichana waliokuwa wakimwangalia kijana kwa sauti
ya chinichini,
“Mm! Vicky unampenda nini?”
msichana mwingine alihoji kwa
sauti ya chini pia kisha wote watatu walicheka kwa sauti huku wakigonganishaa
mikono yao.
Robert alitembea haraka haraka kuelekea
kule alikoitwa, hakuwasikia kabisa wasichana hao kile walichokuwa wakiongea na
wala hakuhisi kwamba wasichana hao walikuwa wakimzungumzia, mbali na yote
hakuwazingatia kabisa, kichwani mwake yeye aliyafikiria mambo yake tu.
“Ndiyo Ndugu Askofu huyu ndio
kijana wetu anaitwa Robert”,
“Sawasawa Ndugu Jackson
anaonekana ni kijana safi sana, karibu kijana”,
“Asante, shikamoo”,
“Marahaba, keti basi”,
“Asante”
Robert alishukuru na kisha kuketi
kama ambavyo alielekezwa, macho yake yote yalimwangalia Askofu huyo
akimsikiliza akiongea
“sasa Ndugu Jackson kijana wako
amepokelewa, ila nafikri hakupata barua ya maelekezo, ni kwamba simu, mikufu na
cheni hatuvihitaji vitu hivyo katika shule yetu, nguo ni zile tu ambazo kijana
atavaa atakapokuwa anaenda likizoni hatuhitaji nguo zozote zaidi ya uniform
tu”.
“Hilo nafikiri halina tatizo
ndugu Askofu”
aliongea Mzee Jackson bila kujua
kwamba ni jinsi gani kauli hiyo ilivyo msononesha kijana wake.
Kwa Robert kutokuwa na simu kwa kipindi chote
atakachokuwa shuleni itakuwa swala gumu sana kwake kwani simu hiyo ndio kitu
pekee alichokuwa akitegemea kitakachoweza kumuunganisha na familia yake kwa
wakati atakapo ikumbuka.
Kichwani mwake aliamini kuishi bila simu kutamfanya
awe katika mazingira magumu mno.
“Sijui itakuwaje du!”
Aliwaza akiwa bado yumo ndani ya ofisi ya hiyo ya Askofu
pamoja na baba yake, baada ya kumaliza mazungumzo hayo na Askofu, Mzee Jackson
aliagana na Askofu na kisha wakatoka ndani ya ofisi hiyo wakiwa na mwanae
ambapo alitakiwa kumuacha Robert ili aungane na wanafunzi wenzake wanaosubiria
usafiri kwa ajili ya kuwapeleka shuleni kwao.
Robert alimsindikiza baba yake
mpaka alipopanda gari. alihuzunika kuona
baba yake anaichukua simu pamoja na begi lake alilowekea nguo pamoja na
makororkoro yake yote na kurudi nalo.
“Ndio unaniacha baba!” aliongea Robert akiwa kama
vile haamini kinachoendelea,
“Ndio mwanangu, najua una wasiwasi, ondoa huo
wasiwasi hayo ni maisha ya kawaida tu”
“Lakini nitawakumbuka sana”
“hilo lisikupe shida, lazima ujifunze maisha ya peke
yako”
aliongea mzee Jackson kwa kumpa moyo kijana wake.
Robert alitabasamu mara baada ya baba yake kumweleza
kauli hiyo lakini macho yake bado yaliendelea kuonyesha huzuni, ilikuwa vigumu
kwake kuyazoea maisha hayo katika mazingira mapya kabisa huku hata watu pia ni
wapya katika macho yake.
“Baki salama mwanangu nakutakia masomo mema”
aliongea Mzee Jackson akiwa amemkumbatia mwanae.
“Nashukuru baba, na wewe nakutakia safari njema”
mara baada ya maongezi hayo Mzee Jackson aliingia
ndani ya gari yake tayari kwa kuanza safari yake. Alipoliwasha tu gari hilo
kilichofuata ni kupungiana mikono mpaka alipotokomea kabisa, alikuwa akielekea
katika Manispaa ya Mbeya, ambapo alipanga kwenda kupumzika ili mapema siku inayofuata
aianze safari ya kurejea jijini Dar es Salaam, ambako anaenda kujumuika na
mkewe pamoja na binti yake.
Upande wa Robert huzuni iliongezeka mara mbili zaidi
pale aliposhuhudia matairi ya gari la baba yake yakianza kusaga ardhi ya mji wa
Tukuyu, alijiona kama kifaranga cha kuku kilichoachwa na mama yake katika pori,
kwa unyonge akajivuta mpaka pale mapokezi mahali ambapo wanafunzi wenzake
walikaa, akakaa kwenye moja ya viti vilivyokuwepo hapo, huku bado mawazo yakiwa
yamejaa kichwani mwake.
Huzuni aliyokuwa nayo ilikuwa kubwa kweli kweli
alitamani hata kulia lakini aliona aibu kufanya hivyo mbele ya wanafunzi
wenzake, hivyo akaona ni bora aendelee kujikaza tu. Akiangalia pande zote
hakuna hata mtu mmoja aliekuwa akimfahamu kati ya waliokuwa ndani ya mapokezi
hivyo jambo hilo lilimnyima raha kupita kiasi, alijikuta anajikalia kimya
pasipo kumwongelesha mtu yoyote.
Nusu saa baadae basi moja jeupe liliingia katika
maegesho ya ofisi hiyo, kwa kusoma maandishi tu Robert aligundua kwamba hilo
ndilo basi la shule.
‘MANOW JUNIOR SEMINARY’
Hivyo ndivyo yalivyosomeka maandishi hayo
yaliyokuwa yameandikwa kwenye ubavu wa
basi hilo. Mara tu baada ya basi hilo kuegeshwa wanafunzi wote waliambiwa
waingie ndani ya basi hilo, Robert alikuwa ni mmoja kati ya wanafunzi walioingia
mapema zaidi katika basi hilo, alikaa siti ya saba upande wa kushoto, siti
ambayo hukaliwa na watu wawili tu, wakati ile ya upande wa kulia hukaliwa na
watu watatu.
“Tuwahi siti ile”
mmoja kati ya wale wasichana watatu alietambulika
kwa jina la Vicky alisikika akiongea huku akinyooshea mkono kwenye moja kati ya
siti za upande wa kulia ambazo zilikuwa bado kukaliwa na watu, alisema hivyo
sababu alitaka wakae siti moja wote watatu ili kuendeleza maongezi yao wakiwa
ndani ya basi hilo.
“Ona Vicky nimekwishawahi hivi”
aliongea msichana tena kati ya wasichana hao huku
akiwa amekalia mwishoni mwa siti hiyo ili kuzuia mtu mwingine kukaa siti hiyo
zaidi ya rafiki zake.
“Safi sana ume………”
Vicky alikatiza kauli hiyo baada ya kuifikia siti
hiyo hali hiyo ilimkuta mara baada ya kuangaza macho yake katika siti ya saba
upande wa kushoto, alimwona Robert akiwa ameketi peke yake katika siti hiyo ya
watu wawili
Akajikuta anaahirisha papo hapo mpango wa kukaa na
rafiki zake siti moja na kuwahi haraka kwenye siti aliyokalia Robert kabla mtu
mwingine hajakaa kwenye siti hiyo.
“Uuh”
Vicky alishusha pumzi kwa nguvu mara baada ya
kufanikisha zoezi hilo la kukaa kwenye siti hiyo, rafiki zake walikwisha gundua
kitu kilichomfanya Vicky aende kukaa kwenye siti hiyo wakabaki wanacheka huku
wakigonganisha mikono yao.
Pamoja na Vicky kushusha pumzi kwa nguvu kiasi kile
Robert hakugeuza kichwa chake kumwangalia Vicky, aliendelea kuangalia dirishani
ambako ndiko alikokuwa anaangalia toka alipo ingia ndani ya basi hilo.
Vicky
hakutaka kuiacha hali ya ukimya kati yao iendelee hata kwa dakika moja,
akaamua kumwongelesha.
“Mambo”
Vicky alisalimia huku akiwa mametoa tabasamu zito
usoni kwake.
Robert aligeuza shingo yake toka huko dirishani alikokuwa
akiangalia mara baada ya kusikia sauti
hiyo nyororo ambayo hata kama ingelisikika kwenye ngoma za masikio ya nyoka
aliyeko pangoni basi lazima angetoka nje, macho yake yalikutana moja kwa moja
na uso wa Vicky uliokuwaumefunikwa na tabasamu zito lililomfanya Robert
apumbazike kwa sekunde kadhaa.
“Nakusalimia”.
Vicky aliongea kwa sauti laini na yenye mnato baada ya kuona
Robert hajajibu salamu yake. Sauti hiyo ililimzindua Robert na kumfanya
ajishtukie kwa vile alivyokuwa na kuona
aibu kuyaangalia macho ya Vicky.
“Ah poa tu”
aliitikia salamu ya Vicky lakini kwa wasiwasi mno na kisha
kugeukia upande wa dirishani tena.
“Naitwa Vicky”
aliongea tena akiwa na lengo lile lile la kutoa ukimya kati
yao huku akiwa ametabasamu alimwangalia Robert ambae bado alikuwa ameangalia
upande wa dirishani, lakini aligeuza sura yake na kumuangalia Vicky mara baada
ya kupata utambulisho wa jina kwa Vicky, alipogeuka tu akakutana tena na
tabasamu la Vicky na kujikuta nae pia anatabasamu.
“Ah Vicky una jina zuri sana”.
“Asante, na wewe unaitwaje?”
“Robert”
“Oh jina zuri sana”
“Asante”
Robert aliongea huku
macho yake yakimgeukia Vicky, Vicky nae alimuangalia Robert lakini kwa
jicho la wizi.
Basi liliendeleza mwendo huku ndani yake zikisikika kelele
za wanafunzi waliokuwa wakicheka kwa furaha huku wakiambizana haya na yale.
Maongezi kati ya Robert na Vicky yaliendelea na kuzidi
kupamba moto, kwa muda huo mfupi, walijikuta wanazoeana kabisa, hali
iliyopelekea Robert aupoteze kabisa upweke aliokuwa nao, pamoja na woga
aliokuwa nao juu ya kwenda sehemu asikokujua na wala kumfahamu mtu yoyote wa
huko. Ucheshi alioonesha Vicky muda huo ulimfanya Robert ajikute katika hali ya
furaha kama alivyokuwa kwao.
“Umetokea wapi Robert”
“Dar”
“Mhm, Tanzania?”
“Kwani hapa wapi”.
“Kule ndio Tanzania sababu kila kitu kiko huko”
“Hamna hata huku ni Tanzania mbona shule nzuri ziko huku”.
“Lakini Ikulu, Vyuo na hata hospitali nzuri ziko Dar, huduma
zote muhimu zipo huko, kule ndio Tanzania bwana”.
“Hapana Vicky hata huku ni Tanzania sio Dar tu”.
Robert aliongea na kisha wote wawili wakaanza kucheka
maongezi kati yao yaliendelea tu na huku bado safari yao ikiendelea basi likiwa
bado katika mwendo.
“Auuh!”
Robert alilalamika baada ya basi kuwarusharusha pale
lilipopita kwenye madimbwi na shimo yaliyokuwepo katika barabara hiyo ya vumbi.
“Hizi ndizo barabara zetu, umeona nimekwambia huku mwishoni
mwa Tanzania”.
“Hamna bwana mbona hata Dar kuna barabara kama hizi”
“Kweli!”
“Ehe, zipo nyingi tu tena”.
“Siamini!”
“Kweli na kwambia:
Aliongea Robert na kisha kutabasamu alimwangalia Vicky na
baadae kuangalia chini kwa sekunde kadhaa na kuyarudisha tena macho yake usoni
kwa Vicky.
“Vipi mbona kimya”
Aliuliza Vicky kwa kudadisi baada ya kuona kama Robert
anataka kuongea jambo lakini anasita,
“Hamna kitu, sina story tena”.
E3
“Kwa nini?”
“Basi tu, labda uongee wewe”
“Niongee nini”
“Chochote”
“Haya chochote”
Vicky aliongea na kisha wote wawili walicheka
“Acha utani Vicky ongea chochote”
“Chochote”
Vicky aliongea tena na wakaanza kucheka tena, walicheka
mfululizo, kicheko chao kilikatika pale basi lilipoanza kuwarusha rusha tena
pale lilipofikia katika eneo lenye mashimo, watu wote ndani ya basi hilo walikuwa
wakilalamikia hali hiyo wakidai wanaumizwa.
lakini Vicky na Robert hawakuongea chochote zaidi ya
kuendeleza tena kicheko chao huku wakigonganisha mikono yao ilikuwa ni furaha
kwao hali hiyo ya kurushwa rushwa na gari tofauti na wanafunzi wenzao
waliokuwemo ndani ya basi hilo ambao walikuwa wakiilalamikia hali hiyo.
“kama rool costal”
“ndio nini”
Ni mchezo wa kupanda kijigari kinachoendeshwa na mashine
linapitia misuko suko yote ya barabara unayoijua wakati mwingine kama mnapata
ajali vile, linaogopesha sana”
“wee! Sasa kwa nini watu wanapanda”
“ kuchezea hatari hiari ukijua hatari hiyo haiwezi
kukuingiza hatarini ni burudani”
“nimeipenda hiyo”
“nini?”
“jinsi ulivyo usema huo mstari,”
“unafurahisha” Robert alicheka kidogo , na mara gari
liliwarusha tena, lakini safari hii hiyo haikudumu.
Ilitlia kabisa mara baada ya basi kufikia sehemu
zilizomwagwa kifusi ilikuwa karibu na shule ya Manow maeneo ya Lwangwa. Mji
mashuhuri kwa soko la gulio na minada.
“Bado kidogo tu tufike”
“Kweli!”
“Yaa”
Aliongea Vicky kwa kujiamini huku akiingiza mkono wake
kwenye begi lake baada ya kufungua zipu ya pembeni mwa begi hilo akachukua
kalamu na karatasi na kuanza kuandika mambo Fulani katika karatasi hiyo. Robert
alibaki anajiuliza nini anachoandika Vicky lakini hakupata jibu.
“ehe chukua”
Vicky aliongea huku akimkabidhi Robert ile karatasi aliyo
kuwa akiiandika
“Ya nini!?”
Akauliza Robert kwa mshangao
“My phone number” (Namba yangu ya simu)
“Your phone number!!” (Namba yako ya simu!!)
Aliongea Robert kwa mshangao
“Yaa”
Vicky aliitikia na kumfanya Robert alibaki ameshangaa
“Nilifikiri haturuhusiwi kuwa na simu!’
“Wanakataza ndio lakini hawana ulinzi mkali”
“Umejuaje”
“Nilisoma hapa masomo ya kompyuta mwaka jana”.
“Ah, kweli?”
“Yaa”
Aliitikia Vicky kwa kujiamini, na kumuacha Robert katika
hali ile ile ya kushangaa na hapo hapo wazo la kupata mwasiliano na familia
yake lilimjia kwamba angeweza kuwasiliana nao kupitia simu ya Vicky,
alipofikiria hilo tu furaha ilimiminika moyoni mwake na kujikuta anashindwa
kulizuia tabasamu lililotokea usoni kwake.
“Vipi mbona unatabasamu”
Aliuliza Vicky alipoiona hali hiyo ya furaha usoni kwa
Bobert
“ah nimefurahi kujua kwamba una simu”
“mhu”
Vicky aliguna kidogo na kisha kujichekesha kidogo
“Na wewe si unayo”
“Hapana sina”
“ah masihara hayo”
“Kweli nakwambia, Askofu kanieleza simu haziruhusiwi hivyo
baba kaichukua na kurudi nayo nyumbani”
“Oh pole sana” aliogea kwa huruma
“Asante”
“Lakini usihofu tutatumia wote hii ya kwangu”
Aliongea Vicky na kumfanya Robert azidi kufurahi kwani
alichokiongea Vicky ndicho alichokuwa anatamani kiwe.
“Nitashukuru sana Vicky, utakuwa umenisaidia kweli!”
“Usijali Robert”
Aliongea Vicky huku akitabasamu na Robert alitabasamu pia,
macho yao yakagongana kwa sekunde kadhaa pasipo yoyote kati yao kuongea
chochote.
“Tumefika!!”
Ilikuwa sauti ya mmoja kati ya wanafunzi waliokuwepo kwenye
basi hilo na kuwafanya wenzake wote wachungulie madirishani na ndio hiyo Sauti
iliyofanya hali ya ukimya kati ya Vicky na Robert itoweke na kujikuta kila
mmoja anayapoteza macho yake usoni kwa mwenzake.
“Kweli tumefika?” aliuliza
“Ehe, ni hapo tu”
Aliongea Vicky huku akiyaonyesha majengo yaliyoonekana
upande wa kushoto wa barabara hiyo.
“Shule nzuri, ona mazingira yake yanavyovutia”
Aliongea Robert huku macho yake yote mawili akiwa
anayaelekeza kwenye shule hiyo, aliona ni mahali pazuri ajabu.
“Sio nzuri kwa
mazingira tu hata taaluma yake ipo juu”
Vicky aliongea akijaribu kuisikia zaidi shule hiyo, basi
lilikwisha ingia kwenye geti ya shule na kuelekea yalipo maegesho ya magari
hapo ndipo liliposimama na baadae wanafunzi wote walishuka huku sura zao
zikionyesha furaha macho nayo yakiwa juu juu kutizama huku na kule katika
mazingira hayo ya shule ya Manow huku Vicky akijaribu kumwelekeza baadhi ya
sehemu, aliendelea kuwa karibu hivyo utafikiri walitoka sehemu moja, mpaka
walipotengana pale kila mmoja alipoelekezwa mwelekeo tofauti na hata hivyo
walipanga kukutana jioni ya siku hiyo ili Robert apate nafasi ya kuwasiliana na
ndugu zake. Ni kwa muda huo waliotengana ndio Vicky alipata nafasi ya kukutana
na rafiki zake ambapo maongezi yao ya kwanza ilikuwa ni juu ya Robert marafiki zake wote wawili walitaka kujua
ameongea nini na Robert
E4
“Tuambe tu shosti mbona unatubania”
“hamna chochote cha maana yani atujaongea chochote kile”
“masihara hayo, Vicky yani hata mapenzi hamjaongelea”
“Mapenzi wapi ,mtu mwenyewe anaonekana yuko mbali na
mapenzi,sijui kwa nini?,lakini nitajua tu jinsi ya kumpanga”
“Lakini unampenda kweli?”
mmoja kati ya marafiki zake Vicky aliuliza,badala kujibu
swali Vicky alianza kucheka rafiki zake wakabaki wanashangaa sababu hawakujua
kitu kinachomchekesha.
“Unacheka nini sasa?”
“Acha kunichekesha Suzy,kweli yule ndio mwanaume wa kupendwa
na mimi?”
Vicky aliongea kwa dharau na kuanza kucheka tena.
“Sasa mbona unataka kuongea nae kuhusu mapenzi!?”
aliuliza tena Suzy kwa mshangao
“Mapenzi wapi nataka nimwingize kwenye kumi na nane zangu nianze
kumchuna pesa,
Si unajua mtoto wa kibopa yule”
“Da hapo utakuwa umecheza kweli au sio Anita”
,aliongea suzy na kumuuliza yule rafiki yao wa tatu kama
wako sambamba.
“kweli”
Anita aliitikia japo kwa kusitasita kisha wote watatu
wakacheka huku wakifurahia mpango ambao Vicky anafikiria kuufanya.
waligonganisha mikono yao na kisha kuendeleza kicheko chao.
Jioni kama ilivyokuwa ahadi yao Vicky na Robert waliweza
kukutana.Jambo la kwanza baada ya salam Robert aliomba kupatiwa simu.
baada ya kumaliza maongezi yake kwenye simu Robert alibaki
na furaha kubwa ambayo ilionekana wazi usoni kwake,
alifurahi sana kuongea na familia yake alijiona kama vile
yupo pamoja nao.
“Umefurahi?”
Vicky alimuuliza wakati Robert akijichekesha peke yake kutokana
na furaha aliyokuwa nayo
“Sana nashindwa jinsi ya kuielezea furaha hii”
“Sasa nataka kuifanya furaha yako iwe mara mbili”
“What?,oh,no way , you can’t Vicky”[Nini?, oh hapana Vicky
huwezi]
Aliongea Robert huku sura ikiwa bado imejawa na furaha
“Sikiliza Robert nasema hivyo sababu jambo moja ambalo
nataka kukueleza leo tena sasa hivi”
“Sasa hivi?”
Robert aliuliza
“ndio”
Vicky aliitikia
“kitu gani hicho?”
Robert aliuliza kwa mshangao huku akimuangalia usoni ambapo
Vicky nae alimkazia macho Robert kweli kweli kama vile mtu mwenye hisia kali na
kisha akaanza kuongea katika hali isiyo kuwa ya utani kabisa.
“Huu ndio ukweli Robert mimi nakupenda, nakupenda kuliko
kitu chochote kile katika hii dunia
naomba uamini nachosema”
Aliongea Vicky bila kusita huku bado akiwa amemkazia macho
Robert, ambae mara baada kusikia kauli hiyo mapigo ya moyo wake yalibadilika na
kuanza kudunda kwa kasi huku tabasamu
lililokuwepo usoni kwake likipotea taratibu, aliitafakari kauli hiyo ambayo
hakutegemea kabisa kuisikia tena toka kwa msichana mrembo kama Vicky.
Hakutegemea kabisa kwamba kuzoeana na
Vicky kungemfanya ajikute kwenye dimbwi la mapenzi hakutegemea kabisa hata kwa
ndoto ya kuwa siku moja angekuwa na msichana mrembo kama Vicky. Tabasamu
lilivamia ghafla usoni kwake na kujikuta anapagawa kwa furaha na kuifanya
furaha yake iongezeke na kuwa mara mbili zaidi ya ile aliyokuwa nayo mwanzo
“Umeweza Vicky umeweza kweli kuizidisha furaha
yangu,nakupenda Vicky nakupenda pia”
Aliongea Robert kwa furaha na kujikuta anamkumbatia Vicky
kwa furaha
“nakupenda sana Robert”,
aliongea vicky
“Hata mimi nakupenda”
Robert alizidi kusisitiza huku bado akiwa amemkumbatia Vicky
huku wakiwa wamejisogeza kwenye giza totoro.
Mapenzi yao yakawa huku kila mmoja akionyesha kupagawa
kabisa na penzi la mwenzake zaidi
ilikuwa kwa Robert ambae alikuwa kama vile mwendawazimu.
Alikuwa tayari kwa lolote alikwisha jitoa mhanga kwa ajili
ya penzi hilo, bila kujua kwamba Vicky hakuwa pamoja bali alikuwa akifanya
maigizo na sio mapenzi ya kweli kama ambavyo Robert alivyokuwa akifikiria.
“Vicky”,
Robert aliita
“Mh”
aliitika
“Nakupenda kuliko kitu chochote kile”
“Hata mimi nakupenda dear”
“Nakuamini na najua utakuwa na mimi siku zote”
“Usihofu kabisa kuhusu hilo,mimi nimezaliwa kwa ajili yako”
“hata mimi kwa ajili yako mpenzi” Robert aliitikia wakiwa
wameketi gizani usiku mmoja,
hakujua chochote kilichoendelea moyoni kwa Vicky ,alichojua
yeye ni kwamba ana bahati kubwa kuwa na msichana mrembo na mwenye uzuri wa aina
yake .hakufahamu kabisa kitu kilicho mvutia Vicky kwake
“am a lukiest man in the world!” ( mimi ni mwanaume mwenye
bahati zaidi ulimwenguni!)
aliwaza Robert akiwa na imani kabisa kwamba amepata zali
kama lile la mentali , bila kujua kwamba yumo ndani ya mtego.
***********-********-*********-*********
Kwa Vicky na marafiki zake furaha ilitawala kitendo cha
Vicky kumpata Rober kilikuwa ni ushindi mkubwa sana kwao.
Sio kwamba walifurahia Vicky kupata mpenzi la hasha bali
kwao uhusiano wa Vicky na Robert, ilikuwa kama vile Vicky amechimba mfereji wa
pesa hivyo pesa zingekuwa zikimjia tu kama mvua.
Na kweli jambo hilo lilifanikiwa kwa kiasi kikubwa kwani
Robert hakujisikia furaha bila kumpatia hela Vicky , aliamini kwamba Vicky ndio
mtu pekee mwenye uhalali wa kutumia
fedha anayotumiwa na wazazi wake aliamini hivyo sababu alimchukulia Vicky kama
ubavu wake sababu yeye ndio msichana pekee katika dunia aliyetokea kumpenda.
Alimpenda sana alimchukulia kama malkia wa moyo wake na
hakutegemea wala kufikiria kwamba
anaweza kumpenda mwanamke mwingine kama anavyo mpenda Vicky.
“I will love you forever baby” (Nitakupenda milele mpenzi)
,aliwaza Robert huku akimwangalia Vicky kwa hisia
kali.aliamini hakuna mwanamke anayeweza kuchukuwa sehemu kubwa ya moyo wake
kama ilivyo kwa Vicky.
Aliamini Vicky ndio msichana pekee anae upendeza moyo .
Hakuja lililopo moyoni kwa Vicky,hakujua kabisa kwamba Vicky anamchukulia yeye kama mpira alioutoboa kwa
sindano ili kuufanya utoe upepo taratibu .hakujua kwamba VICKY
yupo kwake sababu ya pesa na sio mapenzi kama anavyo muongopea.
Siku moja katika makutano yao ya kila siku Vicky alionekana
mnyonge hali hiyo ilimshtua sana Robert
alitaka kitu kilicho mpata mpenzi mpaka awe katika hali hiyo ya huzuni
namna hiyo, hakusita kumuuliza japo alikuwa na wasiwasi sana moyoni,kwa zaidi
ya dakika kumi na tano alikuwa akimbembeleza Vicky ili amweleze ni kitu gani
kinacho mfanya awe katika hali hiyo ya unyonge lakini Vicky alikuwa mgumu kutoa jibu , kitendo hicho kilizidi
kumchanganya Robert na kumfanya azidi kuingiwa na wasiwasi.
Alizidi kumbembeleza lakini ugumu wa Vicky uliendelea hali
ilizidi kuwa mbaya kwa Robert ambae sasa alianza kulengwa na machozi
“Nina matatizo Robert”
mwishoe Vicky aliamua kuongea
“matatizo gani niambie mimi eh ni nini?”
Robert aliuliza kwa sauti ya upole na ya kubembeleza, kwa
kujivuta Vicky akajibu
“Nataka kuuza simu !”
“Uuze simu!! , kwa nini?”
aliuliza Robert kwa mshangao
“Ndio maana nimekueleza kwamba nina matatizo”
“Matatizo gani hayo dear mbona hutaki kunieleza!?”
aliuza Robert kwa sauti ya upole
“We acha tu mpenzi wangu yani makubwa”
“We nieleze tu hata yaweje”
“Nadaiwa shilingi elfu thelathini na suzy ,toka muda mrefu
nilikuwa nikimzungusha lakini leo amenibana anataka nimpe hela yake leo leo”
aliongea Vicky kwa huzuni
“Yani hilo tu ndio linakuumiza kichwa sasa hukunieleza toka
mwanzo!?”,
aliongea Robert kwa mshangao kwani kwani hakuona kwamba hilo
linaweza kuwa tatizo la kumfanya mpenzi wake auzunike kiasi hicho
“Nilijua labda na una mambo yako”
“Mambo yangu yapi Vicky, wewe ndio mambo yangu, shida zako
zote nizakwangu”
aliongea Robert na kumfanya Vicky ainamishe macho yake chini
kwa aibu moyoni dhamiri yake ilimsuta sababu alichokiongea kwa Robert ulikuwa
ni uongo mtupu shida yake ilikuwa pesa tu
“Popote utaponiona ujue nipo kwa ajili yako , nakupenda
Vicky”
aliongea Robert na
kisha kushika kidevu cha Vicky na kumuinua.
macho yao yaligongana Vicky aliyayumbisha macho yake
nakujikuta anagota kwenye mkono wa Robert
alipoziona noti tatu za shilingi elfu kumi kumi zikiwa kwenye mkono
huo.Alihisi mate yamemjaa mdomoni kwa tamaa furahaa ya ghafla ilifurika moyoni
kwake . alishindwa kuongea chochote akabaki akihemahema huku machozi ya furaha
yakimbumbujika.
“It’s for you baby” (Hii ni kwa ajili yako mpenzi)
Robert aliongea kwa sauti kunon’gona huku akimkabidhi Vicky
noti hizo .
Bila kutegemea Vicky alijitupa mwilini kwa Robert nakumkumbatia
huku akiongea maneno mengi mengi ya kimapenzi
“Nakupenda Robert,nakupenda toka moyoni!”
Vicky aliongea maneno hayo yaliyomfanya Robert azidi
kupagawa kwa furaha na kujipa uhakika wa kuwa na Vicky katika maisha yake yote.
******---********---*********---**********--*******
Mapenzi yao yalikuwa wazi sasa karibu kila mwanafunzi wa
shule hiyo alijua kwamba Robert na Vicky ni wapenzi na wako kwenye mapenzi
mazito.
Kasoro Anita na Suzy marafiki wakubwa wa Vicky ndio walijua
ukweli halisi wa penzi hilo, walijua kwamba Vicky yupo kwa Robert sababu ya
pesa.
Penzi liliendelea huku Robert akizidi kupagawishwa na penzi
hilo, karibu muda wote alimfikiria Vicky, alikuwa bado haamini kwamba Vicky
anaamini kwamba yeye anampenda kweli kweli .Alitaka kumsibitishia Vicky juu ya
penzi la dhati lililopo moyoni mwake lakini hakujua angefanya hivyo kwa njia
gani, alipokuwa katika hali hiyo kufikiria ndipo alipopata wazo ambalo aliona
lingeweza kutatua tatizo hilo.
Aliamua kumpigia simu dada yake na kumtambulisha Vicky kwake
aliamini kwa kufanya hivyo angeweza kumfanya aamini kwamba kweli anampenda kwa
dhati.
Ajawahi hata siku moja kumweleza dada yake habari za mapenzi
lakini siku hiyo ilimbidi ilikudhibitisha penzi la dhati alilokuwa nalo kwa
Vicky. Alipiga simu
“Hallow Dada , vipi huko wazima!”.
Aliongea Robert muda mfupi baada ya simu kupokelewa
“Safi tu mdogo wangu ,vipi wewe mzima!?”
ilsikika sauti ya upande wa pili
“Mi mzima tu Dada!”
“Unaendeleaje na masomo?”
“Salama tu Mungu anasaidia,Baba na mama wazima?”
“Wazima tu yani hakuna tatizo kabisa”.
“Dada nina habari mpya”.
“Zipi hizo!?”
“Kuhusu mimi”
“Nini?”.
“Nina mpenzi sasa!”.
“Mpenzi!!!”
“ndio Dada anaitwa Vicky tunapendana sana!”
“Hongera zako”
“Asante, yupo hapa nataka uongee nae”
“mpe simu basi niongee nae wifi yangu”
“haya huyu hapa”
“Shikamoo”
Vicky alisalimia
“Malhaba Vicky hujambo!”
“Sijambo!”
Vicky aliitikia
“Nimefurahi kuku fahamu Vicky , niambie kweli unampenda
mdogo wangu?”
Rehema dada yake Robert aliuliza swali hilo
na kutega sikio lake kwa makini iliasikie jibu atakalopewa
na Vicky
“Ndio dada nampenda sana”
Vicky aliitikia haraka haraka
“Kweli?”
Aliuliza tena
“Kabisa” aliitikia
“Nimefurahi kusikia hivyo, ila naomba uniahidi kitu kimoja”
“kitu gani?”
“Niahidi kwamba hautamuumiza mdogo wangu”
“Nakuahidi”
“ahsante sana”
“Na wewe pia”
“Haya mpe simu Robert”
“Sawa kwaheri”
“Hallow dada”
“Robert japo sijamuona lakini nahisi Vicky ni msichana mzuri
hongera kwa kuchagua”
“Asante dada!”
“Okey bye!” ( sawa kwa heri! )
“Bye!” ( kwa heri )
Robert aliitikia na kisha kukata simu, moyo wake ulikuwa
umejaa furaha tupu,
alifurahishwa sana na kitendo cha Rehema kumfurahia Vicky na
pia alifurahia kitendo cha kufanikisha lengo lake la kumsibitishia Vicky kwamba
kweli anampenda kwa dhati.
“Umeamini vicky umeamini kwamba kweli nakupenda eh!”
“Robert mimi nakuamini , nakuamini kwa asilimia zote naomba
usiwe na wasiwasi kabisa”
“Kweli Vicky!”
“Kabisa”
Vicky aliongea na kisha kumsogelea Robert
“Mwaa!”
alimbusu Robert shavuni, busu hilo lilifika mpaka moyoni kwa
Robert na kumfanya azidi kupagawa na penzi hilo na kujiona yupo katika dunia ya
peke yake , yeye naVicky tu kama ambavyo Adam na Eva walivyokuwa katika bustani
ya Edeni.
Vicky alizidi kufurahi pale alipoona Robert anazidi
kuchanganyikiwa na penzi. Akiamini kwamba hali hiyo ingemfanya awe na uwanja
mpana wa kupata pesa toka Robert ambae alikuwa tayari kuongea kila aina ya
uongo kwa wazazi wake ili waweze kumtumia pesa zaidi ili aweze kumpatia Vicky.
Vicky aliwasimulia rafiki zake juu ya hatua ya Robert
kumtambulisha kwa dada yake
“Nikamwamkia akaitikia ,akasema nimefurahi kukufahamu
,akaniuliza kama kweli nampenda mdogo wake nikamjibu ndio na tena akaniomba
nimuahidi kwamba sito muumiza mdogo wake pia nikamuahidi”
Vicky alimaliza kuongea kauli hiyo na kuanza kucheka ambapo
suzy nae akaanza kucheka pia.
“Umempatia kweli,saizi utakuwa unachuna kotekote”
Suzy aliongea na kisha kuendeleza kicheko pamoja na Vicky.
Tatizo lilikuwa kwa Anita ambae tangu walipoanza mazungumzo
hayo mpaka muda huo yeye alikuwa amebaki kimya tu .kitendo hicho kiliwafanya
Vicky na Suzy wabaki wakimshangaa kwani hiyo haikuwa kawaida yake.
“Vipi Anita mbona hivyo!?”.
Aliuliza Vicky kwa mshangao
“Siwezi kuendelea kuunga mkono huo ubaya wako”
“Ubaya gani !?” ,
Vicky aliuliza huku bado akiwa katika hali ya kushangaa
,hakuelewa kabisa kitu ambacho Anita anakizungumzia.
“Ukatili huo unao mfanyia mtoto wa watu!”
aliongea Anita kwa ukali
“Ukatili!!”.
“Ndio ukatili, huwezi kumchezea mtoto wa watu kiasi hicho”.
“Mbona sikuelewi Anita!?”
“Unielewi nini unavyomuongopea Robert unafikiri huo sio
ukatili eeh, amekukosea nini mtoto watu mpaka umfanyie yote hayo!?”.
Anita aliongea kwa ukali huku Vicky na Suzy wakiwa midomo
wazi kwa mshangao hawakutegemea kabisa kwamba Anita angediriki kuongea maneno
kama hayo mbele yao.
Ilikuwa ni ajabu kweli kwao kwani Anita ni rafiki yao lakini
sasa ameonyesha moyo wa usaliti
“anita kama mimi namuongopea Robert wewe inakuhusu nini?”
aliuliza Vicky kwa ukali
“Hata kama hainihusu lazima nikwambie ukweli umezidi Vicky”
Anita alijibu kwa kufoka, Vicky alifoka na Anita alifoka pia
yani hakukuwa na maelewano kabisa.
“Kama mimi nimezidi sasa wewe sasa inakuhusu nini?”
“Hapana Vick….”
Suzy alimkatisha
“Hapana nini Anita wewe hayo haya kuhusu ni mambo ya Robert
na Vicky we unaongea kama nani?”
Suzy nae alifoka
“Suzy na wewe unamuunga mkono!?”
aliuliza Anita kwa mshangao, alimshangaa Suzy sababu yeye
ndio alikuwa mtu wa kwanza kumteta Vicky karibu kila siku Vicky alipokuwa mbali
nao akidai Vicky anafanya vibaya huku akilaani kitendo hicho lakini ajabu
katika kumweleza Vicky ukweli anaamua kugeuka kama kinyonga na kujifanya yuko
upande wa Vicky
“Sasa kumbe ulifikiri mimi ni msariti kama wewe, unajifanya
rafiki kumbe una lako moyoni mnafiki mkubwa we!”
aliongea Suzy kwa nyodo.
“Na kwa taarifa yako hatuiitaji kampani yako tena na
ukijifanya unaleta kidomodomo chako tuta kufunza adabu!”
Vicky aliongea kauli hiyo kwa ukali akijaribu kumtisha Anita
, sababu alihisi kwamba Anita anaweza kumweleza Robert ukweli. Jambo Vicky hakutaka litokee kabisa kwani
lingemfanya akose hela ambazo alikuwa
anazipata kwa kumchuna Robert. Anita alitishika na maneno ya Vicky sababu
alilijua balaa lake akitibuliwa,ujasiri wote aliokuwa nao ulimwisha akabaki
kimya kwa nukta kadhaa huku uso wake ukionyesha wazi wasiwasi aliokuwano.
Lakini hata hivyo hakutaka kuishia hapo moyo wake ulimsukuma
kuongea zaidi
“Poa tu hata mkinitenga ,lakini mambo hayo lazima yawatokee
puani”.
Aliongea Anita kwa wasiwasi huku akirudi nyuma ambapo
aligeuka nyuma kuanza kuondoka haraka aliogopa kupigwa kwani alijua Vicky ana uwezo
huo .
“Eti yatatutokea puani mjinga kweli huyu!”
aliongea Vicky huku akimcheka Anita ,walicheka pamoja na Suzy huku
wakigonganisha mikono yao hawakujali tena urafiki wao na anita , sababu anita
alishawaasi na kuwasaliti.
***
MWISHO WA KITABU CHA KWANZA
NOT YOU NOW BOOK 01
NOT YOU NOW BOOK 1
{si wewe kwa sasa}
BY D.G.LWASYE 'GIFT KIPAPA'
STORI KWA UFUPI:
Ni stori inayohusu wanafunzi wawili Joel na Grace, hawa walikuwa
wanafunzi waliofanikiwa sana katika taaluma tangu waliposhiriki mashindano ya
kujieleza kwa lugha ya kiingereza katika mdaharo na kuiletea heshima shule yao,
waliishia kuwa wapenzi walioshibana lakini mapenzi yao yanageuka shubiri pale
mmoja wapo alipomaliza shule na kumuacha mwenzie akiendelea, hilo bado alikuwa
jambo lilililo muumiza yoyote kati yao kiasi cha kutosha kama ambavyo aliumia
Grace pale Joel anapomweleza kwamba yeye sio anaye mpenda kwa sasa bali kuna
mtu mwingine. Simulizi hii iliyojaa maumivu ya moyo na kutaabika kwa nafsi
katika kupigania kulipata penzi tena itakusisimua moyo wako kuliko hata
unavyoweza kuvutia picha.
MWANZO:
USHINDI WA UPENDELEO:
Kelele za wanafunzi wa sekondari ya Tukuyu iliyopo wilayani
Rungwe mkonani mbeya, zilisikika wakiwa ndani ya bwalo la shule yao.
Walikuwa hawasiklilizani kabisa kila mmoja aliongea
anachokijua.
Nusu saa iliyopita ndani ya bwalo hilo kulikuwa na
mashindano ya kumtafuta mwanafunzi mwenye uwezo wa kujieleza katika mdahalo wa
lugha ya kiingereza yani Debate.
Mashindano hayo ambayo hatima yake ilikuwa ni
kuwapata washindi wawili , wa kike na wakiume ambao watakwenda
kuiwakilisha shule yao katika mashindano ya wilaya, wakishinda hapo waingie
katika mashindano ya mkoa na baadae mashindano ya kitaifa.
Ushindani huo uliokuwa ukifanyika katika sekondari ya Tukuyu
ulikuwa ukifanyika nchi nzima. Na baadae wangetafuta mkali wa kujieleza kwa
lugha ya kiingereza kwa taifa zima.
Waliofikia fainali ya mashindano hayo katika sekondari ya
tukuyu kwa upande wa wavulana ni .Joel John wa kidato cha tatu na Emanuel
mwambuluma wa kidato cha nne. Na upande wa wasichana ni fatuma abdala wa kidato cha nne na Grace Samson wa kidato
cha kwanza.
Muda wa kuwatangaza washindi ulifika na mwakilishi wa majaji
alisimama na kuanza kutangaza.
“mshindi wetu kwa upande wa wanaume ni Joel John.”
Alitangaza jaji huyo , wanafunzi wote walishangilia na
kupiga vifijo, makofi na ndelemo.
Kwani hakuna mwanafunzi ambaye alikuwa ajui uwezo wa joel
John katika kujieleza kwa lugha ya kiingereza
“haya jamani tulieni tumtangaze mshindi wetu wa kike.”
Aliongea jaji huyo, na kisha wanafunzi wote wlitulia na
kutega sikio , kwani kila mtu alikuwa na hamu ya kumjua mshindi huyo.
Wengine walisikika wakinong’onezana na kulitaja jina la
Grace kwani wengi walishamtabili Grace Samson kuwa ndiye mshindi, kwani pamoja
na kuwa kidato cha kwanza Grace Samson alikuwa na uwezo mkubwa sana wa kuongea
lugha ya kiingereza, aliweza kuyapangilia mawazo yake vizuri kiasi kwamba kila
alipokuwa akiongea katika mashindano hayo watu walikuwa wakimshangila sana na
kumpigia makofi. Alikuwa ni mwanafunzi wa pekee katika shule hiyo kwani
haikuwahi kutokea mwanafunzi wa kidato cha kwanza akawa na uwezo wa kujieleza
na kuzungumza lugha ya kiingereza kiasi hicho.
“Jamani mshindi wetu ni…”
Kabla hata jaji huyo hajaongea watu walidakia na kuongea kwa
sauti.
“GRACE SAMSON.”
“Jamani mimi ndio ninaye tangaza naomba mtulie .”
Jaji huyo aliongea na kisha watu wote wakatulia ili kumsikiliza.
“mshindi wetu ni
Fatuma abdalla.”
Aliongea jaji huyo na kisha kushuka kwenye jukwaa hilo
haraka haraka. Hata mwenyewe alijua amekosea
na ndio maana alishuka haraka. Hakuwa na jinsi hivyo ndivyo ilivyoamliwa
pamoja na majaji wenzake.
“aaah, haiwezekani hiyo.”
Wanafunzi walisikika wakipiga makelele kuonyesha wazi kabisa
kwamba wamepingana na matokeo hayo.
Majaji wote walikwishaondoka ndani ya bwalo hilo kupitia
mlango wa nyuma na kuwaacha wanafunzi wenzao wakipigizana makelele hayo.
Wanafunzi hao waliendelea kupiga makelele hayo huku kila
mmoja akizungumza maneno ya kwake
“haiwezekani lazima tufanye mgomo alisikika mwanafunzi mmoja
akiongea kwa sauti.
“Ndio hapatoshi leo!”
Wenzake waliitikia kwa sauti kubwa. Waliendelea na makelele
huku kila mmoja akidai Grace ndio
anayetakiwa kuwa mshindi.
‘NGLII, NGLIII, NGLIII’
Ilisikika sauti ya kengele. Wanafunzi wote walishangilia
uliposikika mlio huo, ilikuwa ni saaa nane na dakika kumi na tano.
Huo ndio muda ambao wanafunzi wa shule hiyo wanakula
chaskula.
Maongezi yalibadilika na kuwa katika makundi makundi huku
wakitawanyika kuelekea bwenini kwenda kuchukua vyombo vyao vya kulia chakula.
Waliporudi toka huko maongezi yalikuwa mengine kabisa .
Hakuna aliyezungumzia juu ya mdahalo bali ni chakula.
Wengine walilalamika na kuwakaripia wapishi kwa kuwapakulia
chakula kidogo , huku wale wasiokuwa na pesa ya kununulia matunda wakiomba omba
kwa wenzao walionunua.
Na hata baada ya chakula hakuna aliyelifufua suala la
mdahalo bali ilikuwa juu ya mechi kali ya kabumbu ambayo ilitakiwa kucheza kati
ya kidato cha pili na kidato cha nne.
Kila mtu al;ikuwa akimsifia mchezaji wake na huku kila mtu
akitabili ushindi kwa timu aliyoipenda.
Walipokwenda uwanjani huko ndio ilikuwa balaaa, shamla
shamla za mpira zilikuwa zimeshamili kweli kweli. Kuna baadhi ya wanafunzi
walikuwa wakizunguka uwanja mzima wakiimba nyimbo za kuitukuza timu yao huku
wakitupa vijembe na maneno ya kebehi kwa timu pinzani.
Wengine walipiga ngoma na kucheza wanawake wal;ikuwa
wakichweza na wengine walijifunua nguo kabisa kuwa onyeshea utupu timu pinzani,
japo hao walinukuliwa majina yao na kilanja wa nidhamu na waliporudi shule
walikutana adhabu zao.
***
Grace aliumizwa sana na kitendo cha kutotendewa haki na
majaji, moyoni mwake alijisikia kunjwa moyo kupita kiasi, alikuwa
amekwishajiwekea asilimia zote mia kwa mia kwamba yeye ndio mshindi wakike
katika shindano hilo. Alikuwa akijiamini kwa kuwa uwezo wake ulikuwa wazi
kabisa.
Lakini hata hivyo Grace hakutaka kuchukulia suala la
kushindwa kama ni tatizo kubwa sana, kwani hata angeshinda lisingekuwa jambo
ambalo lingemfanya awe na maendeleo mazuri kwenye masiomo yake, hivyo akaamua
kulichukulia suala hilo kama la kawaida tu
Aliamua kusahau kila kitu kuhusu mdahalo na kuweka juhudi
zake katika masomo.
Joel John mshindi wa shindano hilo la mdahalo kwa upande wa
wanaume alikuwa ni mmoja kati ya watu walioguswa sana na suala la majaji
kufanya upendeleao kwa kumchagua fatuma , aliuona uwezo aliokuwa nao fatuma
jinsi ulivyokuwa mdogo ukilinganisha na uwezo wa Grace.
Japo grace alikuwa kidato cha chini.
“hii sio haki wala siwezi kukubali.”
Aliwaza joel alipokuwa ameketi peke yake kwenye kivuli chas
mojakati ya miti iliyokuwepo ndani ya
shule yao. Alikuwa amepania kweli kuiona haki inatendeka na haki anapata nafasi
yake .hakujua kwa nini moyo wake unamsukuma kufanya yote hayo ila alishangaa
kujiona ana kiu ya kutaka kuona Grace anatendewa haki.
BARUA YA JOEL
Alichokifanya Joel ni kuchukua Kalamu na karatasi kisha akaandika barua ya
malalamiko kwa mkuu wa shule, akidai wanafunzi wa kidato cha kwanza
hawajatendewa haki katika mashindano hayo japo walikuwa na uwezo mkubwa.
Alipomaliza kuandika barua hiyo aliikunja vizuri na kuitia katika bahasha.
Usiku muda wakujisomea akaenda mpaka ilipo ofisi ya mkuu wa shule na kuipitisha
barua hiyo chini ya mlango..
Kisha akarudi darasani na kuendelea kujisomea kama wanafunzi
wengine walivyofanya. Japo yeye alisumbulia wa wanafunzi wenzake waliokuja
kwenye dawati yake na kumpa hongera ya ushindi alioupata siku hiyo.
Alishukuru japo moyoni hakuwa na furaha kwani aliamini ushindi huo usingeweza
kukamilika bila ya Grace, alimkubali sana Grace sababu alijua anaweza aliamini
kama wangekuwa pamoja katika mashindano hayo basi wangeweza kuiwakilisha vema
shule yao katika mashindano hayo.
Ahsubuhi siku inayofuata mida ya saa mbili na nusu wanafunzi
wote wakiwa madarasani wakifundishwa na walimu , kengele ililia na kuwashtua
wanafunzi wote kwa sababu kengele hiyo haikiuwa ile ambayo ilipaswa kusikika
kwa wakati huo ambayo ilikuwa ikiashiria kipindi kuisha , bali kengele hii
ilikuwa ile inayoashiria dharula au muda wa masomo kuisha.
Wanafunzi wote walitoka madarasani na kwenda mstalini
haraka ili kujua kile kilicho sababisha
kulia kwa kengele hiyo.
Hakuna aliyejua sababu ya kengele hiyo kulia si kilanja mkuu
wala mgonga kengele mwenyewe yeye alifuata amri tu aliyopewa na mkuu wa shule.
Ni Joel pekee ndio alikuwa ana hisi hisi tu kwamba huenda
ujumbe wake umemfikia mkuu wa shule.
Wanafunzi wote walijipanga kila kidato na mstali wake ,
walikaa kimya ilikujua kinachoendelea.
Jukwaani alisimama mkuu wa shule na mwalimu wa taaluma,
muonekano wa mkuu wa shule uliwatisha wanafunzi wote, uso wake ulikuwa umekunjamana
kwa hasira. Jambo hili lilimfanya joel apate uhakika kwamba sasa ujumbe wake
umefika.
Kilanja mkuu aliitwa na kukabidhiwa karatasi awasomee wenzake kilichoandikwa katika
karatasi hiyo, alianza kusoma.
“kwako mkuu wa shule , shikamoo, mimi ni mwanafunzi wako
naleta malalamiko yangu juu ya jambo alilotendewa mwanafunzi wa kidato cha
kwanza katika mashindano ya kumtafuta mwanafunzi anayeweza kujieleza vizuri
katika mdahalo kwa lugha ya kiingereza.
Grace Samson mwanafunzi wa kidato cha kwanza amejieleza vizuri
sana na ametoa hoja ambazo kama angepewa nafasi ya kuiwakilisha shule yetu
katika mashindano hayo nje ya shule nina hakika angeweza kuleta sifa ambayo kwa
hakika shule yetu ingejivunia kuwa naye, lakini kwa kuwa majaji wa shindano
hilo walikuwa ni wanafunzi wa kidato cha nne basi wameamua kufanya maamuzi
wanavyojua kwa kumpatia mwanafunzi mwenzao wa kidato cha nne aitwaye fatuma
Abdalla nafasi hiyo wakati hana uwezo mkubwa kama ilivyo kwa Grace Samson.
Nimesikitishwa sana
na maamuzi haya mkuu, na nina hoji kwamba kuna haja gani ya wanafunzi wa kidato
cha kwanza kuwekwa kwenye mashindano hayo kama watasimama kama vivuli tu?
Si kawaida kwa shule zetu hizi za serikali ambazo wanafunzi
wake wengi wanatokea shule zetu za msingi ambazo zinatumia lugha ya Kiswahili
kama lugha ya kufundishia kuweza kuzungumza na kujieleza vizuri lugha ya
kiingereza kama ambavyo Grace Samson
ameweza , bali wengi wanakuwa wakitatizwa na lugha hiyo mpaka kufikia kidato
cha pili hadi cha tatu hivi, lakini leo hii mwanafunzi wa kidato cha kwanza
ameonyesha uwezo huo na alichoambulia ni kuvunjwa moyo na kupokonywa haki yake.
Ni hayo tu mkuu nimeandika kwako kwa kuwa najua wewe ndio
mkuu wa shule hii na ndio mwamuzi wa mwisho katika masuala yote yanayoendelea
katika shule hii ili uweze kuliangalia jambo hili na kuhakikisha haki
inatendeka, Ahsante.”
Alimaliza kusoma kilanja mkuu.
Wanafunzi wote walishikwa na bumbuwazi huku wote wakiwa
wamegeuza vichwa vyao kumuangalia Grace kwani kila mmoja aliamini Grace ndio
aliyeandika barua hiyo.
“Ni nani aliyeandika barua hiyo?”
Aliuliza mkuu wa shule , wanafunzi wote walibaki kimya
“narudia tena swali langu , ni nani ameandika barua hiyo?”
Aliuliza tena mkuu wa shule macho ya wanafunzi wote yalikuwa
kwa Grace.
“mimi ndio nimeandika.”
Sauti hiyo iliposikika wanafunzi wote waligeuza vichwa vyao
kumuangalia mtu aliyeitoa kauli hiyo,
hakuna aliyeamini baada ya kumuona Joel akijitokeza.
“Ni Joel!, jamani mungu wangu!”
ilisikika sauti ya msichana mmoja aliyeongea kwa masikitiko, kwani walichoamini wanafunzi wote ni kwamba Joel amefanya kosa kubwa. Ambalo linaweza kumfanya afukuzwe shule au kupewa adhabu kali. Walifikiria hivyo kwa sababu walimfahamu vyema mkuu wao wa shule, alikuwa hapendi mzaha hata kidogo, alikuwa haoni hasara kumfukuza shule mwanafunzi hata kama akifanya kosa hata kidogo, kesi ikimfikia yeye tu basi hakukuwa na msamaha.
ilisikika sauti ya msichana mmoja aliyeongea kwa masikitiko, kwani walichoamini wanafunzi wote ni kwamba Joel amefanya kosa kubwa. Ambalo linaweza kumfanya afukuzwe shule au kupewa adhabu kali. Walifikiria hivyo kwa sababu walimfahamu vyema mkuu wao wa shule, alikuwa hapendi mzaha hata kidogo, alikuwa haoni hasara kumfukuza shule mwanafunzi hata kama akifanya kosa hata kidogo, kesi ikimfikia yeye tu basi hakukuwa na msamaha.
Wapo wanafunzi waliofukuzwa kwa kutovaa tai, soksi na hata
kutochomekea shati sembuse yeye ambaye alifikia hatua ya kumuandikia barua
kabisa.
Joel aliyajua yote hayo lakini tayari alikuwa ameshaamua
kujitoa mhanga, alikuwa tayari hata kufukuzwa shule lakini sio kuiona haki ya
Grace inapotea.
Alijitokeza mbele ya jukwaa, wanafunzi wote walikuwa
wakimuangalia kwa huruma. Upande wa Grace ndio machozi yalikuwa yakimbubujikka
mashavuni , aliumia kuona mtu anataka kufukuzwa shule kwa sababu yake.
Mkuu wa shule alimuangalia Joel na kisha kutoa tabasamu
usoni mwake na tabasamu hilo lilikuwa la kwanza tangua aliposimama katika
jukwaa hilo ahsubuhi hiyo.
“mpigieni makofi.’
Mkuu wa shule aliamrisha, nukta hiyo hiyo wanafunzi wote
walipiga makofi huku wakiwa hawaelewi kwa nini mkuu kawambia wafanye hivyo.
“Vizuri.”
Mkuu wa shule aliongea mara baada ya wanafunzi kumaliza
kupiga makofi hayo.
Alikaa kimya kwa nukta kadhaa na kisha kuanza kuongea tena.
“huyu ni mfano wa kuigwa , katika shule yangu hajawahi
kutokea mwanafunzi mwenye ujasiri na mpenda haki kama ilivyo kwa kijana huyu.”
Aliongea huku akimuangalia Joel usoni alimpa mkono na Joel
aliupokea mkono huo na wakasalimiana kwa mara ya kwanza na mkuu wa shule tangu
aanze masomo yake miaka mitatu iliyopita.
“hongera sana kijana kwa ujasili wako.”
Aliogea mkuu wa shule huku bado wakiwa wameshikana mkono.
“ahsante mkuu.”
Aliitikia Joel japo wasi wasi bado ulikuwa haujatoka mwilini
mwake.
Mkuu wa shule baada ya kumaliza kupeana mkono na Joel,
aliwageukia wanafunzi , ambapo aliwaita majaji wa shindano hilo na kuwakaripia
sana , alimgeukia mwalimu wa taaluma naye pia alimkaripia kwa kuacha tukio
kubwa kama hilo lifanywe na wanafunzi
wenyewe japo yeye alijitetea kwamba alikuwa na dharula iliyompelekea kutofika
kabisa shule siku hiyo.
Hakuishia hapo uongozi wote wa wanafunzi ulikaripiwa
mno. Alimuita Grace mbele akampa pole na
kisha akataka pambano hlo lirudiwe muda huo huo na yeye akiwepo, vipindi pamoja
na shuguli zote za kiofisi zilisimamishwa kwa muda kisha alitaka wanafunzi wote
, walimu pamoja na wafanyakazi wa shule wote wepo katika mpambano huo.
Yani ilikuwa kama baraza la shule ambalo huwa linafanyika
mara moja tu kwa muhula.
MASHINDANO LA HAKI.
Mambo yalionekana hadharani
na kuwafanya ,majaji wa mwanzo waumbuke kwani uwezo wa Grace ulionekana
dhahiri, alifanya vizuri kupita kiasi , na kumuacha Fatuma abdalla akijiuma uma
na kujikanyaga kanyaga, hadi mkuu wa shule alibaki anashangaa ni utumbo gani
huo ulikuwa unaenda kuiwakilisha shule yake katika suala nyeti kama hilo linalo
husu taaluma ya shule.
Wakiwa wameboreka na utumbo aliokuwa akiuwasilisha fatuma
katika mapambano hayo, Joel aliingilia kati
na kusimama upande wa fatuma na kulifanya pambano hilo libadilike na
kuwa ni mashindano ya kujieleza kati ya wavulana na wasichana, hapo kila
mwanafunzi alishangilia kwani hoja zilizokuwa zikitolewa hapo kati ya pande
zote mbili zilikuwa ni moto wa kuotea mbali, Joel akitoa hoja hii , Grace
aliipangua na yeye alitoa ya kwake basi ilikuwa vuta nikuvute kila mwamba ngoma
alikuwa akivutia kwake , kilichotokea hapo ni makofi ndelemo na vifijo toka kwa
wanafunzi , akiongea Grace wasichana wote walishangilia , akiongea joel
wavulana nao walishangilia mjadahalo huo ulikuwa ni wa aina yake katika shule
yao kusema kweli hii ilikuwa ni mara ya kwanza kufanyika mdahalo wenye
washabiki na uliowakosha wanafunzi kama ulivyokuwa mdahalo huo , yani hadi muda
wa kunywa chai uliwapita bila ya wao wenyewe kujua, walikuja kushtuka imefika
saa nane mchana ambapo mkuu wa shule aliingilia kati mjadala huo na kusema
machache.
“Grace Samson na Joel john, kwakweli sijui nieleze ni jinsi
gani ninavyojivuna kuwa na wanafunzi kama nyinyi, katika historia yote ya shule
yetu hatujawahi kutuma timu iliyokamilika kiasi ambacho timu yenu imekamilika,
nina uhakika nyie mnakwenda kuitangaza shule yetu kuliko ilivyowahi kutangazwa
wakati wowote ule.”
Aliongea mkuu wa shule na wanafunzi wote walishangila, hii
ilikuwa ni mara ya kwanza wanafunzi kushangilia wakati mkuu wao akiwa kati kati
ya maongezi, lakini siku hiyo ilitokea na na hata yeye mwenyewe alijikuta
akitabasamu.
Aliongea mengi sana mchana huo na yote yaliwasifia joel
pamoja na grace.
Kilichofuata baada ya hapo alimuagiza mwalimu wa taaluma
kwamba tangu sasa joel na grace wanatakiwa kuandaliwa muda maalumu wa kufanya
mazoezi ya mdahalo , watahilisha masomo yao yote na kuandaliwa timu ya waaalimu
ambayo itakuwa inaandaa midahalo mbali mbali yemnye nguvu na iliyowahi
kufanyika popote afrika mashariki na walimu hao walitakiwa kuwafua kila siku
mpaka siku watakapo enda kupambana na timu
ya shule pinzani, wataandaliwa chakula maalumu na watakuwa wakipata mafunzo hayo kutwa nzima, wakijadili
mijadala mbali mbali katika kila Nyanja ,ziwe za kisiasa , kiuchumi, elimu
historian a Nyanja zingine zote.
Kwa kweli jambo hili lilimfurahisha kila mtu katika
aliyekuwepo hapo hii ilikuwa ni mara ya kwanza kwa sekondari ya tukuyu kuwekeza
nguvu zake katika suala la midahalo, miaka mingine yote suala hilo lilipita
kama upepo na wala hawakujaribu kufika katika hatua yoyote .
Lakini leo kwa ushawishi mkubwa wa uwezo waliuonyesha joel
na Grace wameweza kumshawishi mkuu wa shule yao kuwa na imani nao.
Ilikuwa ni furaha isiyokuwa na kifani katika shule yao hata
majaji waliomnyima nafasi kwa mara ya kwanza walijikuta wakishangilia kama
walivyofanya wanafunzi wenzao huku wakizuga zuga na aibu zao zilizokuwa
zimewajaa usoni.
Hapo ndipo moyo wa Joel ulipotulia kwani alichokitaka
kimekwisha timizika alijisikia amani na furaha tele moyoni kuona Grace amepewa
haki yake na pia alijiona sasa kweli anakwenda kwenye mashindano kwani kwa kuwa
alikuwa na timu iliyokamilika.
Grace Samson upande wa wasichana na joel john upende wa
wavulana kama ilivyokuwa minong’ono ya watu siku za nyuma walipokuwa wakichuana
katika mpambano huo kabla majaji feki hawajaaribu mambo.
Grace akutegemea kabisa kwamba angeipata nafasi hiyo.
Kichwani kwake alikuwa amekwishafuta kabisa suala la mdahalo na kukubali
kushindwa japo haikuwa haki yake.
Lakini leo katika mazingira ambayo hakuyategemea kabisa
amejikuta anashindana upya na fatuma na kunyakuwa ushindi wake wa halali.
Alijisikia faraja sana kuona haki yake iliyukuwa imepotea
sasa imerejea mikononi mwake, moyoni mwake ilijaa furaha tupu ya kupata nafasi
hiyo, hata hivyo hakuona kama furaha yake inaweza kukamilika siku hiyo kama
ahatozitoa shukurani zake za dhati kwa Joel , kwani yeye ndio alikuwa ndio
chanzo cha ushindi huo ambao yuko kuufurahia.
“lazima nimtafute Joel ili nimshukuru.”
Aliwaza grace akiwa bado yumo ndani ya bwalo ambapo kulikuwa
na wanafunzi wenzake lukuki ambao bado walikuwa wakishangilia ushindi ambao
ameupata.
Grace aliyapepesa macho yake karibu kila kona ya ukumbi huo
na hatimaye kufanikiwa kumuona Joel akiwa na wenzake wakicheka na kufurahi kama
walivyofanya wanafunzi wengine katika bwalo hilo.
Grace akaanza kupiga hatua kuelekea pale ambapo joel alikuwa
amesimama.
“Grace !”
mwanafunzi mmoja wa kiume alimuita na kisha Grace aligeuka kumuangalia, alikuwa ni kiche kiche mmoja kati ya wanafunzi wanao sifika sana kwa kucheza kabumbu katika shule hiyo, na ni mwenye rekodi ya kufunga magoli mengi zaidi katika wilaya nzima ya rungwe, japo pia amekuwa na kashfa ya kugombanisha wasichana shuleni hapo kuliko mvulana yoyote Yule.
mwanafunzi mmoja wa kiume alimuita na kisha Grace aligeuka kumuangalia, alikuwa ni kiche kiche mmoja kati ya wanafunzi wanao sifika sana kwa kucheza kabumbu katika shule hiyo, na ni mwenye rekodi ya kufunga magoli mengi zaidi katika wilaya nzima ya rungwe, japo pia amekuwa na kashfa ya kugombanisha wasichana shuleni hapo kuliko mvulana yoyote Yule.
“Hongera sana.”
Aliongea Kiche kiche huku akitabasamu.
“ahsante .”
Grace aliitikia na kisha kutabasamu pia.
Macho yao yaligongana na wakawa wanatazamana kwa sekunde
kadhaa.
“Grace! Grace! Grace! Grace!”
Kiche kiche alianza kuimba huku akipiga makofi , wanafunzi
waliokuwepo jirani nae walimuitikia wakaimba wimbo huo wa kumshangilia Grace
huku wakimzunguka na kumpigia makofi, wengine walipiga vifijo na ndelemo pia.
Grace alionyesha tabasamu lakini moyoni alikereka kwani
kumshangilia kwao kulimfanya achelewe kukutana na Joel kwa wakati huo kama
ambavyo alikuwa amepanga , kwani yeye ndio mtu pekee ambaye kama akisema
hongera moyo wake ungejisikia furaha ya kweli. Na si hawa wengine wanafiki
ambao walibaki kimya siku ya jana wakati haki yake inadhurumiwa.
Dakika tano bnaadae wanafunzi hao walimaliza kumuimbia na
hiyo ni kwa sababu walisikia kengele ya muda wa chakula ikilia , kama
ilivyokuwa jana walisahau habari yote ya Grace na sasa akili zao zilikuwa
zikiwaza chakula tu.
Grace aligeuza macho yake kumuangalia Joel pale alipokuwa
amesimama na rafiki zake muda ule wala hakumuona.
Furaha yote aliyokuwa nayo moyoni ilitoweka na huzuni
ikatanda ghafla sio siri kuvumilia kukukutana na joel hata kwa dakika moja
mbele kulimfanya augue. Hata hivyo hakuwa na jinsi zaidi ya kujipa moyo kwamba
atakutana naye wakati mwingine.
“si yupo hapa hapa shule, nitampata tu.”
Aliwaza na kisha kutoka nje ya bwalo hilo na kwenda kuchukua
chombo cha kulia chakula kama ambavyo walifanya wanafunzi wengine.
Usiku muda wa kujisomea Grace alipata nafasi ya kumuona
Joel, alimkuta akiwa darasani kwao ameketi katikati ya wanfunzi wenzake
akiongoza mjadala wa somo la jiografia.
Grace alisimama
pembeni ya wanfunzi hao alishindwa hata kumuita kwa jinsi alivyokuwa ametingwa
kutoa maelezo kwa wanafunzi wenzake.
yani kama angethubutu kumuomba joel ainuke hapo basi
angeufanya mjadala huo usimame kwa muda. Jambo ambalo kwake aliliona si sawa
ilimbidi atoke nje ili asubiri mpaka mjadala huo uishe lakini alipokuwa akipiga
hatua za kuondoka Joel alimuona.
“Grace !”
Alimuita, Grace alisimama na kugeuka kumuangalia.
“mbona unaondoka?”
Alimuuliza
“nuimeona jinsi ulivyotingwa na mjadala nafikiri ni vizuri
kama nikija baadae.’
“hapana, rafiki zangu wanaweza kusubiri, au sio washkaji?”
“kweli Grace, hata mikiongea saa nzima sisi hatuna noma.”
Aliitikia mmoja kati ya marafiki zake hao na wengine
walitikisa vichwa kuonyesha kwamba wamekubaliana na jambo hilo.
“ila hongera sana Grace!”
Aliongea tena mvulana huyo na kisha Grace alimuitikia ,
wakatoka nje pamoja na joel na kuwaacha rafiki za joel, wakipiga soga zao za
hapa na pale.
PENZI LAIBUKA MOYONI KWA GRACE.
Walienda mpaka kwenye upenu wa darasa hilo , wakasimama hapo
na kuanza rasmi maongezi yao.
“Joel nashindwa hata niseme nini au nikupe nini ili
nionekane kweli nimekupa shukrani za dhati.”
Aliongea Grace huku akimuangalia Joel kwa macho yake ya
kurembua.
“hapana Grace hutakiwi kusema hivyo na wala kuumiza kichwa
kiasi hicho, neno ahsante tu linatosha.”
Aliongea Joel kwa kujiamini huku akimuangalia Grace usoni.
“kweli!?”
Grace aliuliza kwa mshangao
“ndio Grace sitaki kabisa uumize kichwa chako kuliwazia
suala hili.”
“lakini umefanya kazi kubwa Joel.”
Aliongea Grace kwa sauti yake nyororo.
“najua lakini bado nasisitiza ahsante tu inatosha.”
Aliongea Joel kwa msisitizo.
“okey, thanks a lot Joel.”
[ sawa ahsante sana Joel.]
“your welcome.”
[ karibu.]
Joel aliitikia kisha wote wawili waliangaliana huku
wakitabasamu. Zilipita dakika kadhaa wakiwa katika hali hiyo mpaka mwanafunzi
mmoja alipokatiza kwenye upenu huo ndipo walishtuka. Kila mmoja akayapepesa
macho yake na kuangalia sehemu nyingine.
“I have to go now, Grace bye.” [ natakiwa kuondoka sasa ,
kwaheri Grace.]
“okey bye, Joel.” [sawa, kwa heri Joel.]
Grace aliitikia kisha wakashikana mikono ya kuagana ambapo
kila mmoja aliondoka kwa kupita njia yake.
Joel alienda darasani kwao na
kuendelea na majadiliano na wenzake wakati Grace akishuka chini kwenye madarasa
yao.
Alipofika darasani kwao Grace alishindwa kabisa kukaa hata
kwa dakika tano kila alipojaribu kufungua ukurasa wa daftari lake ili asome
hakuna kilichomuingia, alijaribu kuchukua kitabu cha somo lingine ili aone kama
somo hilo litamkubali lakini napo ilikuwa hola , kitabu chake pendwa cha
hadithi kiitwacho mine boy kilichoandikwa na mwandishi nguli wa nchini afrika
ya kuisini Peter Abraham nacho kilimgomea siku hiyo, aliamua kufunga madaftari
yake na kwenda bwenini huko alijitupa
kitandani na kulala chali akiangalia chaga za kitanda cha juu yake.
Mawazo yake yote yalikuwa ni juu ya Joel, mvulana
aliyemfanya apate ushindi katika mashindano ya kumtafuta mwanafunzi anayeweza
kujieleza vizuri kwa kutumia lugha ya kiingereza katika mdahalo.
Kwani bila jitihada za joel, tayari alikwisha tangazwa
ameshindwa.
Japo sifa hizo za joel sio jambo ambalo lilimfanya awe na
mawazo juu yake kwa wakati huo, bali ni kitu kingine kabisa nacho ni mapenzi.
Kuangaika kote kule darasanai mpaka kushindwa kusoma na kuja kujitupa hapa
kitandani huku akigala gala huku na kule katika kitanda hicho ilikuwa ni juu ya
mapenzi, Grace aligundua kwamba anampenda Joel.
“I love him, I real do.”
[ninampenda yeye, kweli ninampenda. ]
Aliwaza Grace huku akiendelea kujigalagaza kitandani.
Jambo hili lili muumiza kichwa kweli kweli kwani pamoja na
uzuri alionao lakini alijiona si kitu bila ya kuwa na Joel. Ugumu ulikuwa ni
jinsi ya kumshawishi Joel kuhusu suala la mapenzi, kwa jinsi alivyoongea nae
muda mchache uliopita hakuonekana ni mtu anayefikiria chochote kuhusu mapenzi.
“sijui nitafanya nini Mungu wangu.”
Aliwaza Grace na kujiuliza maswali ambayo hakupata
majibu yake.
Mapema siku iliyofuata Joel na Grace walifuatwa madarasani
na kupelekwa katika chumba maalumu ambacho huwa kinatumika kufanyia mikutano
mbali mbali ya waalimu.
Huko waliwakuta walimu watano wakiwa wamejipanga na
maandalio yao. Kazi ya kujichua kwaajili ya mdahalo ilianza vilitolewa vichwa
vya maada mbalimbali na wakaanza kuijadili moja baada ya nyingine huku kila mmoja akitoa hoja kulingana na
upande aliopangiwa uwe ni upande wa kupinga hoja au upande wa kuikubali,
wakichuana vikali huku waalimu hao wakiwasaidia pale walipotoka nje ya mstali
na pia waliwasaidia namna ya kujenga hoja zilizo na mashiko walifanya hivyo mpaka ulipofika muda wa
mapumziko ambapo chai yao waliletewa humo humo walikunywa na kupewa muda mchache
wa kupumzika na kisha shughuli iliendelea ilikuwa ni hoja juu ya hoja
walinolewa hivyo kwa muda wa juma zima mpaka muda wa jioni ambao walikuwa
wakiutumia kwa ajili ya kujisomea nao pia waliutumia kwa kazi hiyo hiyo.
Waliendelea hivyo hivyo mpaka ilipofika siku ya mpambano wa
kumtafuta mwakilishi wa willaya, ambapo shule zote za wilaya ya rungwe
zilishiriki na katika mpambano huo walitakiwa kumtafuta mwakili mmoja wa
kiume na mmoja wa kike katika wilaya
nzima haijalishi anatokea shule gani. Ili waiwakilishe wilaya yao katika ngazi
ya mkoa na baadae ngazi ya taifa kama wakifanikiwa kuvuka ngazi ya mkoa.
Kama kawaida Joel na grace walitakiwa kuiwakilisha shule yao
katika mashindano hayo.
Mpambano ulianza na ulikuwa moto kweli kweli na mwishowe
ulifika muda wa kuwatangaza washindi wa mpambano huo ambapo walianza kumtanga
za mshindi upande wa wanaume.
“Joel John ndiyo mwakilishi wetu wa wilaya kwa upande wa
wanaume.’
Ilisikika sauti hiyo ya jaji ikimtangaza Joel kuwa ndio
mshindi , wanafunzi wa shule ya tukuyu sekondari walishangilia kupita kiasi.
Ikafika zamu ya kumtangaza mshindi wa kike.
Wanafunzi wote walitulia na kutega masikio yao kwa makini.
“Grace Samson, kutoka tukuyu sekondari.”
Jaji huyo alimtangaza Grace hapo sasa wanafunzi wa shule ya
tukuyu sekondari walikuwa kama vile wendawazimu kwa furaha, waliimba , wariruka
na kushangilia huku wakikimbaia kuelekea
shuleni kwao.
Grace na Joel walikuwa wamebebwa juu juu huku wakiimba wimbo
uliotaja majina yao na kuwasifia .
Joel alijisikia fahari kubwa kuwa shujaaa wa shule yake,
hiyo ilikuwa ni heshima kubwa kwa shule yao tangu kuanzishwa kwa mashindano
hayo shule yao haikuwahi kuwa wawakilishi
wa wilaya.
Lakini leo imewezekana tena kwa kuchukua nafasi zote
mbili ya kike na ya kiume
Jambo ambalo hakuna shule iliyowahi kulifanya hapo kabla,
ilikuwa kama mvulana akitokea shule hii basi msichana anatokea shule nyingine.
Lakini leo imekuwa kinyume kabisa kwani nafasi zote mbili zimechukuliwa na
tukuyu sekondari.
USHINDI WA MKOA.
Grace nae alikuwa na furaha kupita kiasi alifurahia ushindi
mkubwa walioupata nae pia aliamini kwamba hicho ni kitendo cha kishujaa sana
kwa shule yake.
Alifurahia kuiwakilisha shule na wilaya yake katika mashindo
hayo ya mdahalo wa lugha ya kiingereza .
Lakini furaha yake ilikuwa na dosari moyoni mwake, kwani
bado hakuona kama furaha hiyo imekamilika.
Alitamani furaha hiyo ingemkuta akiwa kwenye mapenzi na
joel.
Alimpenda sana Joel na alitamani kumuona joel analiona penzi
alilonalo kwake ili wawe pamoja katika hali ya kupendana.
“Grace.”
Grace aliisikia sauti hiyo iliyomfanya azinduke toka kwenye
mawazo aliyokuwa nayo.
Aligeuza shingo lake kumuangalia mtu aliyemuita.
Hakuweza kuamini pale alipokutana na tabasamu zito la
joel, mapigo yake ya moyo alianza kubadilika
na kuanza kwenda kwa kasi, akajikuta ameduwaa na kumuangalia joel.
“hongera Grace.”
Aliongea Joel huku akitabasamu.
Grace kabla ajaongea chochote alimsogelea joel na
kumkumbatia.
“hongera na wewe joel.”
“asante .”
Aliitikia.
“lakini yote hii ni kwa sababu yako bila wewe nisingefika
hapa.”
“mmmh,mmhh, usiseme hivyo, umefanya juhudi grace , unafikiri
ni watu wangapi wamefikia hatua hiyo lakini hawajaweza kushinda.”
“ni kweli joel lakini wewe ndio chanzo cha yote.”
“sawa lakini unajua tumeipa heshima kubwa sana shule yetu.”
“sana.”
“sio sana Grace bado tuna safari ndefu ngazi ya mkoa na
taifa zinatusubiri.”
“unafikiri tutafika taifa kweli?”
Grace aliuliza .
“tukisimama hivi wawili , kamwe hatuwezi kuzuilika.”
Aliongea joel kwa kujiamini , kisha wote walicheka.
Walikuwa wakiongea maongezi hayo
huku bado wanafunzi wenzao wakiwa shangilia.
Waliporudi shule pamoja na kushangiliwa vile lakini bado
walirudi tena kambini kunolewa safari hii walifuliwa mpaka saa tano za usiku,
wakiwa na walimu wao watano ambao walikuwa wakiwa pika na kuwa fua ile ile walitoa hoja na kujibiza na siku nzima huku
wakisubiri tarehe ya kwenda mkoani kuchuana na wanafunzi wengine waliokuwa
wakiziwakilisha wilaya zao zipatazo nane zinazoujenga mkoa wa mbeya. Japo
maandalizi ya nguvu kama ambayo walikuwa wakiyafanya washindani toka sekondari
ya tukuyu yalikuwa hayafanywi na shule nyingine yoyote kwanza hata umoja hawakuwa nao kila mshindani
alitoka shule yake na baadhi walitoka katika shule walizokuwa mahasimu hivyo
kichwani mwa kila mmoja alikuwa akifikiria jinsi ya kumshinda mwenzake angalau
kuchukua namba ya juu kuliko yeye na wengine ile kuwa mmoja kati ya watu kumi
na sita bora toka katika shule zote za
mkoa wa mbeya alikuwa sifa tosha kabisa .
Aliona ufahari kukaa katika hoteli kubwa akihudumiwa na
serikali kula chochote akipendacho hadi kufikia siku ya pambano.
Muda wa kuwatafuta wanafunzi wawili watakao uwakilisha mkoa
wa mbeya katika mashindano ya mdahalo wa lugha ya kiingereza utakao fanyika
kitaifa ulitimia.
Wanafunzi kumi na sita kutoka katika shule mbali mbali za
mkoa wa mbeya kati yao wakiwemo grace na joel kutoka sekondari ya tukuyu
walikuwa tayari kwa ajili ya mapambano hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa
mbeya sekondari.
Mpambano mkali ulifanyika huku kila mmoja akijitahidi kadiri
ya uwezo wake kujitutumua kila awezavyo kutema ung’eng’e ili mradi aibuke
kidedea katika mashindano hayo na mwisho wa yote washindi wa mashindano hayo
walitangazwa
Joel na grace Ndio walioibuka kidedea katika mashindanio
hayo, wao ndio waliotakiwa kuuwakilisha mkoa wao katika mashindano hayo ya
kitaifa yatakayofanyika katikak jiji la Dar es salaam.
Wakiwa pamoja na mwalimu wao wa taaluma waliruka ruak na
kushangilia kwa furaha baada ya kufanikiwa kupata nafasi hiyo ilikuwa ni furaha
isiyokuwa na kifani kwao hawakutegemea kabisa kwamba jambo hilo lingewezekana
pamoja na kufanya juhudi zote zile, hiyo ilikuwa kama ndoto kwao.
“siamini kabisa Joel.”
Aliongea grace.
“Hata mimi Grace,”
Joel aliitikia wakiwa wamekumbatiana wakifurahia ushindi
wao.
Mwalimu wao wa taaluma alikuwa amesimama pembeni yao nae pia
uzalendo ulimshinda akajikuta nae pia ameungana kukumbatiana na wanafunzi wake
kwa furaha, sio siri ushindi wa grace na joel ulimfurahisha kupita kiasi , hii
itakuwa ni mara yake ya kwanza kupata safari ya kikazi kwenda makao makuu ya
elimu tangu aanze kazi. Tena kwenda
makao makuu akiwa mwalimu wa wanafunzi wanaoweza kujieleza vizuri zaidi kwa
kutumia lugha ya kiingereza katika mkoa mzima wa mbeya.
Alijua jinsi ambavyo jambo hilo litaipa sifa shule yake na
hata yeye pia kama mwalimu wa taaluma.
“mmenifurahisha sana , matumaini yangu mtafanya vivyo hivyo
katika mashindano ya kitaifa.”
Aliongea mwalimu kwa furaha.
“bila shaka mwalimu.”
Joel aliitikia.
“kweli kabisa , Mungu yuopo pamoja nasi , lazima tushinde.”
Grace nae pia aliomngea na kisha waliendelea kushangilia
ushindi huo huku wakiimba wimbo wa kuisifushule yao, waalimu pamoja na wanafunizi wa shule hiyo.
Siku hiyo kwao ilikuwa ni furaha kweli kweli .
Wale wanafunzi wa shule zingine
walioshindwa wakabaki wakiwashangaa tu.
Moyoni mwa Grace bado kulikuwa na kasoro , furaha yake bado
ilikuwa haijakamilika pamoja na ushindi wote huo walioupata , bado akilini
mwake alikuwa akifikiria juu ya joel, alimpemnda na alitaka joel alitambue
jambo hilo.
Lakini hakuwa na ujasiri wa kumweleza juu ya vile
anavyojisikia juu yake.
Aliogopa kumweleza kwamba anampenda sababu alikuwa na wasi
wasi kwamba joel anaweza kuwa na hisia tofauti juu ya jambo hilo, kwa kweli
suala hilo liliusononesha moyo wake.
“Vip Grace mbona umekuwa kimya hivyo?”
aliuliza Joel mara baada ya kuona Grace amepona kwa muda mrefu.
aliuliza Joel mara baada ya kuona Grace amepona kwa muda mrefu.
Swali hilo lilimfanya Grace azinduke toka kwenye mawazo
mazito aliyokuwa nayo.
Moyoni mwake aliisikia sauti ikimwambia,
“mweleze ukweli
anaweza kukuelewa, huyo ni mvulana,
wavulana huwa hawana tabia ya
kukataa wasichana wazuri kama wewe.”
“niambie Grace una tatizo gani.”
Joel aliongea kauli ambayo ilikuwa ikimtaka Grace kuongea
kile kinachomtatiza kama vile ambavyo mawazo yake yalimtaka afanye .
“ah, hamna tatizo Joel .”
Aliongea Grace haraka haraka
na kujichekesha ili aoneakane kweli hana tatizo.
“sawa nilijua labda una tatizo kwa sababu nilikuona kimya muda mrefu.”
“hapana joel zaidi tu
nina furaha kutokana na ushindi tulioupata, kama ulivyoseam joel tukisimama pamoja , hakuna kitakachoweza
kutuzuia.”
Aliongea grace kisha wote wawili
walitabasamu. Grace hakuwa na maana ya kuwa pamoja katika mashindano ya
mdahalo, bali pamoja daima na milele
katika maisha, alitaka kuwa na joel katika kipindi chote cha maisha yake
na hakutaka kuzuiwa na chochote kumpata Joel.
SAFARI YA DAR ES SALAM
Kilichofuata baada ya joel na Grace kushinda mashindano hayo
ya kumtyafuta mwanafunzi anayeweza kujieleza vizuri katika mdahalo wa
kiingereza kwa ngazi ya mkoa sasa walitakiwa kusafiri mpaka jijini Dar es
salaam, mahali ambapo mashindano ya kumtafuta mshindi wa mashindano hayo
kitaifa yalifanyika. Waliingia katika jiji hilo na kufikia katika hoteli ya
kifahari iliyokatika ufukwe wa bahari ya hindi
Sea cliff hotel, huko waligharamiwa kila kitu na serikali. Wao ilikuwa
ni kufurahia maisha tu.
Ilikuwa ni jambo la furaha sana kwa Joel na Grace kukaa
ndani ya hoteli kubwa kiasi hicho ndani kulikuwa na kila kitu , vinywaji vya
kila aina, bafuni bafu lilikuwa na maji ya vugu vugu na ya baridi pamoja na
jakuzi na mambo mengine kibao ambayo ni ya a hadhi ya nyota tano.
Joel alifurahi kupita kiasi kwa sababu hakuwahi kuota hata
siku moja kwamba atakuja kuingia kwenye hoteli ya kifahari kiasi hicho sio yeye
tu hata grace pia nae alikuwa na furaha moja ya ajabu mwalimu wao ndio usiseme
yeye ndio alikuwa kama chizi muda wote alishinda kwenye jakuzi. Hata habari ya
kuwa simamia joel na Grace ili wafanye mazoezi kama ambavyo alikuwa
akiwasimamia wakati wapo mkoani kwao hiyo hakuwa nayo, alikuwa akikamua mitungi
iliyokuwa kwenye friji mpaka iliimba haleluya.
“unajisikiaje kuwepo hapa, Grace?”
aliuliza joel huku akiwa ametabasamu.
aliuliza joel huku akiwa ametabasamu.
“vizuri sana , natamani maisha yetu yote yangekuwa hapa.”
Aliongea Grace na kisha Joel
akacheka.
“maisha yetu yote!?”
Jole aliuliza.
Jole aliuliza.
“Ndio Joel tuishi humu tukiwa tunahudumiwa na wahudumu kama
malkia na mfalme .”
Aliongea Grace maneno hayo kwa hisia , kwa sababu alikuwa
akiyaongea maneno hayo toka moyoni mwake.
“kwa nini umesema malkia na mfalme?”
Aliuliza Joel huku akimuangalia Joel usoni.
Swali hilo lilimshtua Grace alianza kuwa na wasiwasi kwamba
pengine Joel ameshashtukia kwamba yeye anampenda. Japo alipenda jambo hilo
litokee lakini alikuwa na hofu nalo kwani hakujua joel angelipokea vipi, mapigo
ya moyo wake yalibadilika na kuanza kudunda kwa kasi sababu ya woga .
“mbona unijibu Grace?”
Aliuliza joel na kumfanya Grace azidi kuwa na wasi wasi,
alishindwa kabisa kufungua mdomo na kulitolea maelezo jambo hilo.
“sababu nakupenda.”
Aliwaza Grace kichwani mwake hilo ndilo jibu pekee alilokuwa
likimjia kichwani mwake kila alipofikiria kumjibu Joel. Lakini alikosa ujasiri wa kufungua mdomo wake
na kutoa jibu hilo.
Joel hakujua chochote kilichoendelea moyoni mwa Grace na wala hakuhisi jambo lolote hadi
wakati huo.
“Grace!”
Joel aliita baaada ya kimya kirefu kilichokuwepo baada ya
joel kushindwa kujibu swali ambalo joel alimuuliza.
“mmh”
Aliitikia grace kwa woga, bado alikuwa na wasi wasi
alifikiria bado joel anasubiri jibu kutoka kwake.
“hivi itakuwaje kama tukuishinda?”
aliuliza joel na kumfanya Grace atokwe na hofu aliyokuwea nayo na kurudi katika hali yake ya kawaida.
aliuliza joel na kumfanya Grace atokwe na hofu aliyokuwea nayo na kurudi katika hali yake ya kawaida.
“nitafurahi joel yani siwezi hata kuelezea jinsi furaha
yangu itakavyokuwa.”
Aliongea grace kwa
hisia.
“n a kama ukishinda wewe peke yako?”
Joel aliuliza tena.
Joel aliuliza tena.
“siwezi kufurahi joel , siwezi kufurahi hata kidogo , siwezi
kufurahi wakati wewe umeshindwa, nataka tushinde wote Joel na kama kushidwa basi tushindwe wote.”
“kwa nini?”
“kwa sababu sisi ni wa moja joel , tumetoka mkoa mmoja ,
wilaya moja , na shule moja.”
“lakini madarasa tofauti.”
Aliongea joel kwa utani
na kisha wote wawili walicheka,.
“hata kama madarasa
mawili tofauti joel lakini mimi na wewe ni wa moja.’
“kivipi?”
Joel aliuliza.
“kumbuka wewe ndio uliyefanya mpaka mimi nikashiriki
mashindano haya, unafikiri kama tusinge kuwa wa moja ungeweza kuipigania nafsi
yangu kiasi kile , unafikiri ungeweza kujitoa mhanga kwa ajili yangu, unafikiri
ungeweza kweli.?”
Grace aliongea maneno hayo kwa hisia huku joel akiwa kimya
kumsikiliza kwa makini, Alishindwa kabisa kuongea chochote maneno aliyoongea
grace yaliugusa kweli moyo wake,
alijikuta anapoteza tabasamu alilokuwa nalo usoni mwake na kuyafikiria
maneno ya Grace , japo hakujua grace alimaanisha nini kuongea maneno hayo.
Akili yake ilirudisha nyuma mawazo na kukumbuka jinsi
alivyompigania grace mpaka kufanikisha aingie katika mashindano hayo.
Lilikuwa ni jambo lililohitaji ujasiri wa hali ya juu na
hata kumuingiza katika hatari ya
kufukuzwa shule lakini yeye bila kujali kufukuzwa shule wala lolote lile alijikuta
anafanya jambo hilo kwa ajaili ya Grace, sio kwa ajili yake bali kwa ajili ya
Grace.
“Grace ni nani kwangu?”
aliwaza Joel na kuwazua lakini hakupata jibu lolote kichwani mwake , kusema kweli hadi wakati huo alikuwa hajui lolote lililomfanya mpaka apigane kiasi hicho kwa ajili ya msichana huo.
aliwaza Joel na kuwazua lakini hakupata jibu lolote kichwani mwake , kusema kweli hadi wakati huo alikuwa hajui lolote lililomfanya mpaka apigane kiasi hicho kwa ajili ya msichana huo.
“nikisema nilitaka kuona haki ikiitendeka, mbona nimewahi
kushuhudia watu wengi wakidhurumiwa haki zao lakini kamwe sikuwahi kuwa
hangaikia? Kwa nini nilisimama kwa sababu ya Grace , Grace ni nani kwangu?”
Alizidi kuwaza Joel na mawazo hayo yalizidi kumuumiza
kichwa.
“Joel vipi, mbona umekuwa kimya hivyo?”
aliuliza Grace kwa mshangao baada ya kuona Joel amebadilika ghafla.
aliuliza Grace kwa mshangao baada ya kuona Joel amebadilika ghafla.
“Grace nahitaji kuwa peke yangu kwa wakati huu, tafadhari
naomba uniruhusu niende chumbani kwangu.”
Aliongea Joel mara baada ya kuona mambo yamemzidia.
Grace alishangazwa na kauli hiyo na wala hakuitegemea.
MWISHO WA KITABU CHA KWANZA
Subscribe to:
Posts (Atom)