BY D.G.LWASYE 'GIFT KIPAPA'
Mwanzoni mwa mwaka 2000, mwaka
ambao haukuwa mpya peke yake bali pia ulikuwa ni mwanzo wa karne mpya ya
ishirini na moja. Watu walikuwa wana tarajia mambo mengi sana mwaka huo ikiwa
pamoja na vitisho kama vile mwisho wa dunia na kutokufanya kazi kwa kompyuta,
yote hayo yalikuwa ni chachu zilizoufanya mwaka huo uwe wa kipekee.
Katika ofisi ya makao makuu ya dayosisi ya mbeya
iliyo chini ya dhehebu la kirutheli, kulikuwa na vijana wengi wa rika moja
waliokuwa wamekaa katika mapokezi ya ofisi hiyo iliyopo katika wiliya ya
tukuyu.
Vijana hao walikuwa ni wanafunzi wapya wa shule ya sekondari iitwayo
‘MANOW JUNIOR SEMINARY’
inayomilikiwa na dayosisi hiyo.
Walikuwa hapo wakisubiri basi la shule liwapeleke
mahali ilipo shule yao ili wakaanze masomo yao ya sekondari kwa mara ya kwanza.
Japo wengi wao walikuwa hawafahamiani lakini
wakajikuta wanazoeana katika kipindi hicho kifupi walichokuwa hapo. Waliongea
na kucheka pamoja kwa ujumla wote walikuwa na furaha ya kwenda kujiunga na
masomo ya sekondari hasa hasa sekondari ya bweni, kwani kwao yalikuwa ni maisha
mapya waliokuwa wakiyaota pindi
walipokuwa shule ya msingi, wakiamini kwamba wakiwa bweni watakuwa huru na sheria na miiko ya wazazi
wao.
Waliongea mambo mengi lakini zaidi ni juu ya maisha
ya bweni , kila mmoja aliongea kile alichowahi kusikia kuhusu bweni.
Wengine walisema
wanafunzi wa vidato vya juu wanawatesa na kuwatumikisha wanafunzi wa
kidato cha kwanza huku wengine wakisema hayo yalikuwa ni mambo ya kizamani ,
siku hizi hakuna anyeingilia uhuru wa mwenzake.
“piiii!, piiii!”
Ilisikika honi toka kwenye gari moja la kifahari
aina ya hammer lililokuwa likiingiia katika maegesho ya ofisi hiyo.
Wanafunzi watatu wa kike ndio waliokuwa wakipigiwa
honi hiyo. Walikuwa wamesimama katika maegesho hayo wakipiga stori mpaka
kujisahau. Walisogea pembeni huku wakicheka, waliliangalia gari hilo lililokuwa
na vioo vyeusi yenye uwezo wa kumzuia mtu wa nje asione ndani ya gari.
Matairi ya gari hilo yalisimama mara baada ya
kuegeshwa vizuri katika maegesho hayo kisha mlango wa upande wa dereva
ulifunguliwa na kisha mtu aliyekuwa akiendesha alishuka.
Sura za wale mabinti waliokuwa wakilikodolea gari
hilo zilibadilika ghafla na kujawa na taharuki hata kicheko chao kilikatika,
hakuna yoyote kati yao aliyeamini kile alichokiona.
Hii ilikuwa ni kwa mara ya kwanza kwao kumuona
mvulana wa rika lao akiendesha gari la kifahari namna hiyo, na haikuwa juu ya
gari peke yake bali pia mavazi yake, cheni
pamoja na saa ya mkononi, kila kitu kilikuwa ni ghari ni kama vile walimuona
nyota wa muziki hip hop nchini marekani.
Sekunde chache baada ya kijana
huyo kushuka mlango wa upande wa pili ulifunguliwa ambapo alishuka mzee mmoja
wa makamo alievalia suti ya rangi ya kahawia. mara baada ya kushuka toka ndani
ya gari hilo, mzee huyo aliliangalia jengo la ofisi hiyo kisha akatabasamu,
akaanza kupiga hatua kuelekea ulipo mlango wa ofisi hiyo ambapo yule kijana
aliyekuwa nae alimfuata.
Wale wasichana watatu waliendelea
kumkodolea macho kijana huyo mpaka alipotokomea ndani ya ofisi hizo.
“Mambo ya vibopa hayo!”
aliongea mmoja kati ya wasichana hao akimaanisha mambo ya
matajiri, wenzake hawakuongea jambo lolote zaidi ya kucheka na baada ya muda
mfupi waliendelea na maongezi yao waliyokuwa wakiongea mawanzoni na kusahau
habari za yule kijana, waliendelea kuongea huku wakicheka na kufurahi.
“Unaona basi nikamwambia huwezi kuju…………”,
msichana huyo alikatiza kile alichokuwa akiwaeleza
wenzake na kisha ukimya ulitawala kati yao kwa muda fulani huku wote watatu
wakiwa makini na kitu fulani, hii iliwatokea mara baada ya kijana yule aliepita
wakati ule, akitoka ndani ya ofisi na kutembea kwa mwendo wa taratibu kuelekea
kule alikoegesha gari yao, ukimya uliendelea kuwapo kati ya wasichana hao huku
macho yao yakimnyemelea kijana huyo.
Kijana huyo ambaye kwa muonekano
hakuwa na sura yenye mvuto wala macho yenye kuvutia sana wasichana, yeye
alikuwa wa kawaida sana kiasi cha kuweza hata kudharaulika hata mbele za
msichana yeyote yule mwenye kuumbika, kifupi mvulana huyo alikuwa mbaya wa sura na
hata umbo, lakini cha ajabu wasichana hao walionekana kumkodolea macho kupita
kiasi mpaka kufikia hatua ya kusitisha maongezi yao.
Mvulana huyo alienda moja kwa moja lilipo gari lao
na kuliegamia na kisha kutoa simu iliyokuwepo mfukoni mwake na kupiga namba
fulani. Wasichana wale watatu waliacha midomo wazi kwa mshangao baada ya kuiona
simu ya mvulana huyo ambayo ilikuwa ni simu ya gharama sana kiasi cha wasichana
hao kutowahi kuiona maishani mwao.
“Vipi sister” alianza kuongea
kijana huyo mara baada ya simu aliyokuwa akipiga kupokelewa.
“Tumefika salama tu, ila uchovu
tu” aliendelea kuongea kijana huyo huku bado wale wasichana wakiendelea
kumwangalia,
“Robert Jackson!” aliita mama
mmoja aliyekuwa amesimama kwenye mlango wa kuingilia kwenye ofisi hiyo, kauli
hiyo ilimfanya kijana yule akate simu hata bila ya kuagana vizuri na aliyekuwa
akiongea nae.
“Naam” kijana yule aliitika akiwa
amesimama wima.
“Unahitajika kwenye ofisi ya
Askofu” aliongea mama huyo mara tu akageuka na kuingia ndani ya ofisi hiyo.
“Kumbe anaitwa Robert Jackson”
aliongea mmoja kati ya wale wasichana waliokuwa wakimwangalia kijana kwa sauti
ya chinichini,
“Mm! Vicky unampenda nini?”
msichana mwingine alihoji kwa
sauti ya chini pia kisha wote watatu walicheka kwa sauti huku wakigonganishaa
mikono yao.
Robert alitembea haraka haraka kuelekea
kule alikoitwa, hakuwasikia kabisa wasichana hao kile walichokuwa wakiongea na
wala hakuhisi kwamba wasichana hao walikuwa wakimzungumzia, mbali na yote
hakuwazingatia kabisa, kichwani mwake yeye aliyafikiria mambo yake tu.
“Ndiyo Ndugu Askofu huyu ndio
kijana wetu anaitwa Robert”,
“Sawasawa Ndugu Jackson
anaonekana ni kijana safi sana, karibu kijana”,
“Asante, shikamoo”,
“Marahaba, keti basi”,
“Asante”
Robert alishukuru na kisha kuketi
kama ambavyo alielekezwa, macho yake yote yalimwangalia Askofu huyo
akimsikiliza akiongea
“sasa Ndugu Jackson kijana wako
amepokelewa, ila nafikri hakupata barua ya maelekezo, ni kwamba simu, mikufu na
cheni hatuvihitaji vitu hivyo katika shule yetu, nguo ni zile tu ambazo kijana
atavaa atakapokuwa anaenda likizoni hatuhitaji nguo zozote zaidi ya uniform
tu”.
“Hilo nafikiri halina tatizo
ndugu Askofu”
aliongea Mzee Jackson bila kujua
kwamba ni jinsi gani kauli hiyo ilivyo msononesha kijana wake.
Kwa Robert kutokuwa na simu kwa kipindi chote
atakachokuwa shuleni itakuwa swala gumu sana kwake kwani simu hiyo ndio kitu
pekee alichokuwa akitegemea kitakachoweza kumuunganisha na familia yake kwa
wakati atakapo ikumbuka.
Kichwani mwake aliamini kuishi bila simu kutamfanya
awe katika mazingira magumu mno.
“Sijui itakuwaje du!”
Aliwaza akiwa bado yumo ndani ya ofisi ya hiyo ya Askofu
pamoja na baba yake, baada ya kumaliza mazungumzo hayo na Askofu, Mzee Jackson
aliagana na Askofu na kisha wakatoka ndani ya ofisi hiyo wakiwa na mwanae
ambapo alitakiwa kumuacha Robert ili aungane na wanafunzi wenzake wanaosubiria
usafiri kwa ajili ya kuwapeleka shuleni kwao.
Robert alimsindikiza baba yake
mpaka alipopanda gari. alihuzunika kuona
baba yake anaichukua simu pamoja na begi lake alilowekea nguo pamoja na
makororkoro yake yote na kurudi nalo.
“Ndio unaniacha baba!” aliongea Robert akiwa kama
vile haamini kinachoendelea,
“Ndio mwanangu, najua una wasiwasi, ondoa huo
wasiwasi hayo ni maisha ya kawaida tu”
“Lakini nitawakumbuka sana”
“hilo lisikupe shida, lazima ujifunze maisha ya peke
yako”
aliongea mzee Jackson kwa kumpa moyo kijana wake.
Robert alitabasamu mara baada ya baba yake kumweleza
kauli hiyo lakini macho yake bado yaliendelea kuonyesha huzuni, ilikuwa vigumu
kwake kuyazoea maisha hayo katika mazingira mapya kabisa huku hata watu pia ni
wapya katika macho yake.
“Baki salama mwanangu nakutakia masomo mema”
aliongea Mzee Jackson akiwa amemkumbatia mwanae.
“Nashukuru baba, na wewe nakutakia safari njema”
mara baada ya maongezi hayo Mzee Jackson aliingia
ndani ya gari yake tayari kwa kuanza safari yake. Alipoliwasha tu gari hilo
kilichofuata ni kupungiana mikono mpaka alipotokomea kabisa, alikuwa akielekea
katika Manispaa ya Mbeya, ambapo alipanga kwenda kupumzika ili mapema siku inayofuata
aianze safari ya kurejea jijini Dar es Salaam, ambako anaenda kujumuika na
mkewe pamoja na binti yake.
Upande wa Robert huzuni iliongezeka mara mbili zaidi
pale aliposhuhudia matairi ya gari la baba yake yakianza kusaga ardhi ya mji wa
Tukuyu, alijiona kama kifaranga cha kuku kilichoachwa na mama yake katika pori,
kwa unyonge akajivuta mpaka pale mapokezi mahali ambapo wanafunzi wenzake
walikaa, akakaa kwenye moja ya viti vilivyokuwepo hapo, huku bado mawazo yakiwa
yamejaa kichwani mwake.
Huzuni aliyokuwa nayo ilikuwa kubwa kweli kweli
alitamani hata kulia lakini aliona aibu kufanya hivyo mbele ya wanafunzi
wenzake, hivyo akaona ni bora aendelee kujikaza tu. Akiangalia pande zote
hakuna hata mtu mmoja aliekuwa akimfahamu kati ya waliokuwa ndani ya mapokezi
hivyo jambo hilo lilimnyima raha kupita kiasi, alijikuta anajikalia kimya
pasipo kumwongelesha mtu yoyote.
Nusu saa baadae basi moja jeupe liliingia katika
maegesho ya ofisi hiyo, kwa kusoma maandishi tu Robert aligundua kwamba hilo
ndilo basi la shule.
‘MANOW JUNIOR SEMINARY’
Hivyo ndivyo yalivyosomeka maandishi hayo
yaliyokuwa yameandikwa kwenye ubavu wa
basi hilo. Mara tu baada ya basi hilo kuegeshwa wanafunzi wote waliambiwa
waingie ndani ya basi hilo, Robert alikuwa ni mmoja kati ya wanafunzi walioingia
mapema zaidi katika basi hilo, alikaa siti ya saba upande wa kushoto, siti
ambayo hukaliwa na watu wawili tu, wakati ile ya upande wa kulia hukaliwa na
watu watatu.
“Tuwahi siti ile”
mmoja kati ya wale wasichana watatu alietambulika
kwa jina la Vicky alisikika akiongea huku akinyooshea mkono kwenye moja kati ya
siti za upande wa kulia ambazo zilikuwa bado kukaliwa na watu, alisema hivyo
sababu alitaka wakae siti moja wote watatu ili kuendeleza maongezi yao wakiwa
ndani ya basi hilo.
“Ona Vicky nimekwishawahi hivi”
aliongea msichana tena kati ya wasichana hao huku
akiwa amekalia mwishoni mwa siti hiyo ili kuzuia mtu mwingine kukaa siti hiyo
zaidi ya rafiki zake.
“Safi sana ume………”
Vicky alikatiza kauli hiyo baada ya kuifikia siti
hiyo hali hiyo ilimkuta mara baada ya kuangaza macho yake katika siti ya saba
upande wa kushoto, alimwona Robert akiwa ameketi peke yake katika siti hiyo ya
watu wawili
Akajikuta anaahirisha papo hapo mpango wa kukaa na
rafiki zake siti moja na kuwahi haraka kwenye siti aliyokalia Robert kabla mtu
mwingine hajakaa kwenye siti hiyo.
“Uuh”
Vicky alishusha pumzi kwa nguvu mara baada ya
kufanikisha zoezi hilo la kukaa kwenye siti hiyo, rafiki zake walikwisha gundua
kitu kilichomfanya Vicky aende kukaa kwenye siti hiyo wakabaki wanacheka huku
wakigonganisha mikono yao.
Pamoja na Vicky kushusha pumzi kwa nguvu kiasi kile
Robert hakugeuza kichwa chake kumwangalia Vicky, aliendelea kuangalia dirishani
ambako ndiko alikokuwa anaangalia toka alipo ingia ndani ya basi hilo.
Vicky
hakutaka kuiacha hali ya ukimya kati yao iendelee hata kwa dakika moja,
akaamua kumwongelesha.
“Mambo”
Vicky alisalimia huku akiwa mametoa tabasamu zito
usoni kwake.
Robert aligeuza shingo yake toka huko dirishani alikokuwa
akiangalia mara baada ya kusikia sauti
hiyo nyororo ambayo hata kama ingelisikika kwenye ngoma za masikio ya nyoka
aliyeko pangoni basi lazima angetoka nje, macho yake yalikutana moja kwa moja
na uso wa Vicky uliokuwaumefunikwa na tabasamu zito lililomfanya Robert
apumbazike kwa sekunde kadhaa.
“Nakusalimia”.
Vicky aliongea kwa sauti laini na yenye mnato baada ya kuona
Robert hajajibu salamu yake. Sauti hiyo ililimzindua Robert na kumfanya
ajishtukie kwa vile alivyokuwa na kuona
aibu kuyaangalia macho ya Vicky.
“Ah poa tu”
aliitikia salamu ya Vicky lakini kwa wasiwasi mno na kisha
kugeukia upande wa dirishani tena.
“Naitwa Vicky”
aliongea tena akiwa na lengo lile lile la kutoa ukimya kati
yao huku akiwa ametabasamu alimwangalia Robert ambae bado alikuwa ameangalia
upande wa dirishani, lakini aligeuza sura yake na kumuangalia Vicky mara baada
ya kupata utambulisho wa jina kwa Vicky, alipogeuka tu akakutana tena na
tabasamu la Vicky na kujikuta nae pia anatabasamu.
“Ah Vicky una jina zuri sana”.
“Asante, na wewe unaitwaje?”
“Robert”
“Oh jina zuri sana”
“Asante”
Robert aliongea huku
macho yake yakimgeukia Vicky, Vicky nae alimuangalia Robert lakini kwa
jicho la wizi.
Basi liliendeleza mwendo huku ndani yake zikisikika kelele
za wanafunzi waliokuwa wakicheka kwa furaha huku wakiambizana haya na yale.
Maongezi kati ya Robert na Vicky yaliendelea na kuzidi
kupamba moto, kwa muda huo mfupi, walijikuta wanazoeana kabisa, hali
iliyopelekea Robert aupoteze kabisa upweke aliokuwa nao, pamoja na woga
aliokuwa nao juu ya kwenda sehemu asikokujua na wala kumfahamu mtu yoyote wa
huko. Ucheshi alioonesha Vicky muda huo ulimfanya Robert ajikute katika hali ya
furaha kama alivyokuwa kwao.
“Umetokea wapi Robert”
“Dar”
“Mhm, Tanzania?”
“Kwani hapa wapi”.
“Kule ndio Tanzania sababu kila kitu kiko huko”
“Hamna hata huku ni Tanzania mbona shule nzuri ziko huku”.
“Lakini Ikulu, Vyuo na hata hospitali nzuri ziko Dar, huduma
zote muhimu zipo huko, kule ndio Tanzania bwana”.
“Hapana Vicky hata huku ni Tanzania sio Dar tu”.
Robert aliongea na kisha wote wawili wakaanza kucheka
maongezi kati yao yaliendelea tu na huku bado safari yao ikiendelea basi likiwa
bado katika mwendo.
“Auuh!”
Robert alilalamika baada ya basi kuwarusharusha pale
lilipopita kwenye madimbwi na shimo yaliyokuwepo katika barabara hiyo ya vumbi.
“Hizi ndizo barabara zetu, umeona nimekwambia huku mwishoni
mwa Tanzania”.
“Hamna bwana mbona hata Dar kuna barabara kama hizi”
“Kweli!”
“Ehe, zipo nyingi tu tena”.
“Siamini!”
“Kweli na kwambia:
Aliongea Robert na kisha kutabasamu alimwangalia Vicky na
baadae kuangalia chini kwa sekunde kadhaa na kuyarudisha tena macho yake usoni
kwa Vicky.
“Vipi mbona kimya”
Aliuliza Vicky kwa kudadisi baada ya kuona kama Robert
anataka kuongea jambo lakini anasita,
“Hamna kitu, sina story tena”.
E3
“Kwa nini?”
“Basi tu, labda uongee wewe”
“Niongee nini”
“Chochote”
“Haya chochote”
Vicky aliongea na kisha wote wawili walicheka
“Acha utani Vicky ongea chochote”
“Chochote”
Vicky aliongea tena na wakaanza kucheka tena, walicheka
mfululizo, kicheko chao kilikatika pale basi lilipoanza kuwarusha rusha tena
pale lilipofikia katika eneo lenye mashimo, watu wote ndani ya basi hilo walikuwa
wakilalamikia hali hiyo wakidai wanaumizwa.
lakini Vicky na Robert hawakuongea chochote zaidi ya
kuendeleza tena kicheko chao huku wakigonganisha mikono yao ilikuwa ni furaha
kwao hali hiyo ya kurushwa rushwa na gari tofauti na wanafunzi wenzao
waliokuwemo ndani ya basi hilo ambao walikuwa wakiilalamikia hali hiyo.
“kama rool costal”
“ndio nini”
Ni mchezo wa kupanda kijigari kinachoendeshwa na mashine
linapitia misuko suko yote ya barabara unayoijua wakati mwingine kama mnapata
ajali vile, linaogopesha sana”
“wee! Sasa kwa nini watu wanapanda”
“ kuchezea hatari hiari ukijua hatari hiyo haiwezi
kukuingiza hatarini ni burudani”
“nimeipenda hiyo”
“nini?”
“jinsi ulivyo usema huo mstari,”
“unafurahisha” Robert alicheka kidogo , na mara gari
liliwarusha tena, lakini safari hii hiyo haikudumu.
Ilitlia kabisa mara baada ya basi kufikia sehemu
zilizomwagwa kifusi ilikuwa karibu na shule ya Manow maeneo ya Lwangwa. Mji
mashuhuri kwa soko la gulio na minada.
“Bado kidogo tu tufike”
“Kweli!”
“Yaa”
Aliongea Vicky kwa kujiamini huku akiingiza mkono wake
kwenye begi lake baada ya kufungua zipu ya pembeni mwa begi hilo akachukua
kalamu na karatasi na kuanza kuandika mambo Fulani katika karatasi hiyo. Robert
alibaki anajiuliza nini anachoandika Vicky lakini hakupata jibu.
“ehe chukua”
Vicky aliongea huku akimkabidhi Robert ile karatasi aliyo
kuwa akiiandika
“Ya nini!?”
Akauliza Robert kwa mshangao
“My phone number” (Namba yangu ya simu)
“Your phone number!!” (Namba yako ya simu!!)
Aliongea Robert kwa mshangao
“Yaa”
Vicky aliitikia na kumfanya Robert alibaki ameshangaa
“Nilifikiri haturuhusiwi kuwa na simu!’
“Wanakataza ndio lakini hawana ulinzi mkali”
“Umejuaje”
“Nilisoma hapa masomo ya kompyuta mwaka jana”.
“Ah, kweli?”
“Yaa”
Aliitikia Vicky kwa kujiamini, na kumuacha Robert katika
hali ile ile ya kushangaa na hapo hapo wazo la kupata mwasiliano na familia
yake lilimjia kwamba angeweza kuwasiliana nao kupitia simu ya Vicky,
alipofikiria hilo tu furaha ilimiminika moyoni mwake na kujikuta anashindwa
kulizuia tabasamu lililotokea usoni kwake.
“Vipi mbona unatabasamu”
Aliuliza Vicky alipoiona hali hiyo ya furaha usoni kwa
Bobert
“ah nimefurahi kujua kwamba una simu”
“mhu”
Vicky aliguna kidogo na kisha kujichekesha kidogo
“Na wewe si unayo”
“Hapana sina”
“ah masihara hayo”
“Kweli nakwambia, Askofu kanieleza simu haziruhusiwi hivyo
baba kaichukua na kurudi nayo nyumbani”
“Oh pole sana” aliogea kwa huruma
“Asante”
“Lakini usihofu tutatumia wote hii ya kwangu”
Aliongea Vicky na kumfanya Robert azidi kufurahi kwani
alichokiongea Vicky ndicho alichokuwa anatamani kiwe.
“Nitashukuru sana Vicky, utakuwa umenisaidia kweli!”
“Usijali Robert”
Aliongea Vicky huku akitabasamu na Robert alitabasamu pia,
macho yao yakagongana kwa sekunde kadhaa pasipo yoyote kati yao kuongea
chochote.
“Tumefika!!”
Ilikuwa sauti ya mmoja kati ya wanafunzi waliokuwepo kwenye
basi hilo na kuwafanya wenzake wote wachungulie madirishani na ndio hiyo Sauti
iliyofanya hali ya ukimya kati ya Vicky na Robert itoweke na kujikuta kila
mmoja anayapoteza macho yake usoni kwa mwenzake.
“Kweli tumefika?” aliuliza
“Ehe, ni hapo tu”
Aliongea Vicky huku akiyaonyesha majengo yaliyoonekana
upande wa kushoto wa barabara hiyo.
“Shule nzuri, ona mazingira yake yanavyovutia”
Aliongea Robert huku macho yake yote mawili akiwa
anayaelekeza kwenye shule hiyo, aliona ni mahali pazuri ajabu.
“Sio nzuri kwa
mazingira tu hata taaluma yake ipo juu”
Vicky aliongea akijaribu kuisikia zaidi shule hiyo, basi
lilikwisha ingia kwenye geti ya shule na kuelekea yalipo maegesho ya magari
hapo ndipo liliposimama na baadae wanafunzi wote walishuka huku sura zao
zikionyesha furaha macho nayo yakiwa juu juu kutizama huku na kule katika
mazingira hayo ya shule ya Manow huku Vicky akijaribu kumwelekeza baadhi ya
sehemu, aliendelea kuwa karibu hivyo utafikiri walitoka sehemu moja, mpaka
walipotengana pale kila mmoja alipoelekezwa mwelekeo tofauti na hata hivyo
walipanga kukutana jioni ya siku hiyo ili Robert apate nafasi ya kuwasiliana na
ndugu zake. Ni kwa muda huo waliotengana ndio Vicky alipata nafasi ya kukutana
na rafiki zake ambapo maongezi yao ya kwanza ilikuwa ni juu ya Robert marafiki zake wote wawili walitaka kujua
ameongea nini na Robert
E4
“Tuambe tu shosti mbona unatubania”
“hamna chochote cha maana yani atujaongea chochote kile”
“masihara hayo, Vicky yani hata mapenzi hamjaongelea”
“Mapenzi wapi ,mtu mwenyewe anaonekana yuko mbali na
mapenzi,sijui kwa nini?,lakini nitajua tu jinsi ya kumpanga”
“Lakini unampenda kweli?”
mmoja kati ya marafiki zake Vicky aliuliza,badala kujibu
swali Vicky alianza kucheka rafiki zake wakabaki wanashangaa sababu hawakujua
kitu kinachomchekesha.
“Unacheka nini sasa?”
“Acha kunichekesha Suzy,kweli yule ndio mwanaume wa kupendwa
na mimi?”
Vicky aliongea kwa dharau na kuanza kucheka tena.
“Sasa mbona unataka kuongea nae kuhusu mapenzi!?”
aliuliza tena Suzy kwa mshangao
“Mapenzi wapi nataka nimwingize kwenye kumi na nane zangu nianze
kumchuna pesa,
Si unajua mtoto wa kibopa yule”
“Da hapo utakuwa umecheza kweli au sio Anita”
,aliongea suzy na kumuuliza yule rafiki yao wa tatu kama
wako sambamba.
“kweli”
Anita aliitikia japo kwa kusitasita kisha wote watatu
wakacheka huku wakifurahia mpango ambao Vicky anafikiria kuufanya.
waligonganisha mikono yao na kisha kuendeleza kicheko chao.
Jioni kama ilivyokuwa ahadi yao Vicky na Robert waliweza
kukutana.Jambo la kwanza baada ya salam Robert aliomba kupatiwa simu.
baada ya kumaliza maongezi yake kwenye simu Robert alibaki
na furaha kubwa ambayo ilionekana wazi usoni kwake,
alifurahi sana kuongea na familia yake alijiona kama vile
yupo pamoja nao.
“Umefurahi?”
Vicky alimuuliza wakati Robert akijichekesha peke yake kutokana
na furaha aliyokuwa nayo
“Sana nashindwa jinsi ya kuielezea furaha hii”
“Sasa nataka kuifanya furaha yako iwe mara mbili”
“What?,oh,no way , you can’t Vicky”[Nini?, oh hapana Vicky
huwezi]
Aliongea Robert huku sura ikiwa bado imejawa na furaha
“Sikiliza Robert nasema hivyo sababu jambo moja ambalo
nataka kukueleza leo tena sasa hivi”
“Sasa hivi?”
Robert aliuliza
“ndio”
Vicky aliitikia
“kitu gani hicho?”
Robert aliuliza kwa mshangao huku akimuangalia usoni ambapo
Vicky nae alimkazia macho Robert kweli kweli kama vile mtu mwenye hisia kali na
kisha akaanza kuongea katika hali isiyo kuwa ya utani kabisa.
“Huu ndio ukweli Robert mimi nakupenda, nakupenda kuliko
kitu chochote kile katika hii dunia
naomba uamini nachosema”
Aliongea Vicky bila kusita huku bado akiwa amemkazia macho
Robert, ambae mara baada kusikia kauli hiyo mapigo ya moyo wake yalibadilika na
kuanza kudunda kwa kasi huku tabasamu
lililokuwepo usoni kwake likipotea taratibu, aliitafakari kauli hiyo ambayo
hakutegemea kabisa kuisikia tena toka kwa msichana mrembo kama Vicky.
Hakutegemea kabisa kwamba kuzoeana na
Vicky kungemfanya ajikute kwenye dimbwi la mapenzi hakutegemea kabisa hata kwa
ndoto ya kuwa siku moja angekuwa na msichana mrembo kama Vicky. Tabasamu
lilivamia ghafla usoni kwake na kujikuta anapagawa kwa furaha na kuifanya
furaha yake iongezeke na kuwa mara mbili zaidi ya ile aliyokuwa nayo mwanzo
“Umeweza Vicky umeweza kweli kuizidisha furaha
yangu,nakupenda Vicky nakupenda pia”
Aliongea Robert kwa furaha na kujikuta anamkumbatia Vicky
kwa furaha
“nakupenda sana Robert”,
aliongea vicky
“Hata mimi nakupenda”
Robert alizidi kusisitiza huku bado akiwa amemkumbatia Vicky
huku wakiwa wamejisogeza kwenye giza totoro.
Mapenzi yao yakawa huku kila mmoja akionyesha kupagawa
kabisa na penzi la mwenzake zaidi
ilikuwa kwa Robert ambae alikuwa kama vile mwendawazimu.
Alikuwa tayari kwa lolote alikwisha jitoa mhanga kwa ajili
ya penzi hilo, bila kujua kwamba Vicky hakuwa pamoja bali alikuwa akifanya
maigizo na sio mapenzi ya kweli kama ambavyo Robert alivyokuwa akifikiria.
“Vicky”,
Robert aliita
“Mh”
aliitika
“Nakupenda kuliko kitu chochote kile”
“Hata mimi nakupenda dear”
“Nakuamini na najua utakuwa na mimi siku zote”
“Usihofu kabisa kuhusu hilo,mimi nimezaliwa kwa ajili yako”
“hata mimi kwa ajili yako mpenzi” Robert aliitikia wakiwa
wameketi gizani usiku mmoja,
hakujua chochote kilichoendelea moyoni kwa Vicky ,alichojua
yeye ni kwamba ana bahati kubwa kuwa na msichana mrembo na mwenye uzuri wa aina
yake .hakufahamu kabisa kitu kilicho mvutia Vicky kwake
“am a lukiest man in the world!” ( mimi ni mwanaume mwenye
bahati zaidi ulimwenguni!)
aliwaza Robert akiwa na imani kabisa kwamba amepata zali
kama lile la mentali , bila kujua kwamba yumo ndani ya mtego.
***********-********-*********-*********
Kwa Vicky na marafiki zake furaha ilitawala kitendo cha
Vicky kumpata Rober kilikuwa ni ushindi mkubwa sana kwao.
Sio kwamba walifurahia Vicky kupata mpenzi la hasha bali
kwao uhusiano wa Vicky na Robert, ilikuwa kama vile Vicky amechimba mfereji wa
pesa hivyo pesa zingekuwa zikimjia tu kama mvua.
Na kweli jambo hilo lilifanikiwa kwa kiasi kikubwa kwani
Robert hakujisikia furaha bila kumpatia hela Vicky , aliamini kwamba Vicky ndio
mtu pekee mwenye uhalali wa kutumia
fedha anayotumiwa na wazazi wake aliamini hivyo sababu alimchukulia Vicky kama
ubavu wake sababu yeye ndio msichana pekee katika dunia aliyetokea kumpenda.
Alimpenda sana alimchukulia kama malkia wa moyo wake na
hakutegemea wala kufikiria kwamba
anaweza kumpenda mwanamke mwingine kama anavyo mpenda Vicky.
“I will love you forever baby” (Nitakupenda milele mpenzi)
,aliwaza Robert huku akimwangalia Vicky kwa hisia
kali.aliamini hakuna mwanamke anayeweza kuchukuwa sehemu kubwa ya moyo wake
kama ilivyo kwa Vicky.
Aliamini Vicky ndio msichana pekee anae upendeza moyo .
Hakuja lililopo moyoni kwa Vicky,hakujua kabisa kwamba Vicky anamchukulia yeye kama mpira alioutoboa kwa
sindano ili kuufanya utoe upepo taratibu .hakujua kwamba VICKY
yupo kwake sababu ya pesa na sio mapenzi kama anavyo muongopea.
Siku moja katika makutano yao ya kila siku Vicky alionekana
mnyonge hali hiyo ilimshtua sana Robert
alitaka kitu kilicho mpata mpenzi mpaka awe katika hali hiyo ya huzuni
namna hiyo, hakusita kumuuliza japo alikuwa na wasiwasi sana moyoni,kwa zaidi
ya dakika kumi na tano alikuwa akimbembeleza Vicky ili amweleze ni kitu gani
kinacho mfanya awe katika hali hiyo ya unyonge lakini Vicky alikuwa mgumu kutoa jibu , kitendo hicho kilizidi
kumchanganya Robert na kumfanya azidi kuingiwa na wasiwasi.
Alizidi kumbembeleza lakini ugumu wa Vicky uliendelea hali
ilizidi kuwa mbaya kwa Robert ambae sasa alianza kulengwa na machozi
“Nina matatizo Robert”
mwishoe Vicky aliamua kuongea
“matatizo gani niambie mimi eh ni nini?”
Robert aliuliza kwa sauti ya upole na ya kubembeleza, kwa
kujivuta Vicky akajibu
“Nataka kuuza simu !”
“Uuze simu!! , kwa nini?”
aliuliza Robert kwa mshangao
“Ndio maana nimekueleza kwamba nina matatizo”
“Matatizo gani hayo dear mbona hutaki kunieleza!?”
aliuza Robert kwa sauti ya upole
“We acha tu mpenzi wangu yani makubwa”
“We nieleze tu hata yaweje”
“Nadaiwa shilingi elfu thelathini na suzy ,toka muda mrefu
nilikuwa nikimzungusha lakini leo amenibana anataka nimpe hela yake leo leo”
aliongea Vicky kwa huzuni
“Yani hilo tu ndio linakuumiza kichwa sasa hukunieleza toka
mwanzo!?”,
aliongea Robert kwa mshangao kwani kwani hakuona kwamba hilo
linaweza kuwa tatizo la kumfanya mpenzi wake auzunike kiasi hicho
“Nilijua labda na una mambo yako”
“Mambo yangu yapi Vicky, wewe ndio mambo yangu, shida zako
zote nizakwangu”
aliongea Robert na kumfanya Vicky ainamishe macho yake chini
kwa aibu moyoni dhamiri yake ilimsuta sababu alichokiongea kwa Robert ulikuwa
ni uongo mtupu shida yake ilikuwa pesa tu
“Popote utaponiona ujue nipo kwa ajili yako , nakupenda
Vicky”
aliongea Robert na
kisha kushika kidevu cha Vicky na kumuinua.
macho yao yaligongana Vicky aliyayumbisha macho yake
nakujikuta anagota kwenye mkono wa Robert
alipoziona noti tatu za shilingi elfu kumi kumi zikiwa kwenye mkono
huo.Alihisi mate yamemjaa mdomoni kwa tamaa furahaa ya ghafla ilifurika moyoni
kwake . alishindwa kuongea chochote akabaki akihemahema huku machozi ya furaha
yakimbumbujika.
“It’s for you baby” (Hii ni kwa ajili yako mpenzi)
Robert aliongea kwa sauti kunon’gona huku akimkabidhi Vicky
noti hizo .
Bila kutegemea Vicky alijitupa mwilini kwa Robert nakumkumbatia
huku akiongea maneno mengi mengi ya kimapenzi
“Nakupenda Robert,nakupenda toka moyoni!”
Vicky aliongea maneno hayo yaliyomfanya Robert azidi
kupagawa kwa furaha na kujipa uhakika wa kuwa na Vicky katika maisha yake yote.
******---********---*********---**********--*******
Mapenzi yao yalikuwa wazi sasa karibu kila mwanafunzi wa
shule hiyo alijua kwamba Robert na Vicky ni wapenzi na wako kwenye mapenzi
mazito.
Kasoro Anita na Suzy marafiki wakubwa wa Vicky ndio walijua
ukweli halisi wa penzi hilo, walijua kwamba Vicky yupo kwa Robert sababu ya
pesa.
Penzi liliendelea huku Robert akizidi kupagawishwa na penzi
hilo, karibu muda wote alimfikiria Vicky, alikuwa bado haamini kwamba Vicky
anaamini kwamba yeye anampenda kweli kweli .Alitaka kumsibitishia Vicky juu ya
penzi la dhati lililopo moyoni mwake lakini hakujua angefanya hivyo kwa njia
gani, alipokuwa katika hali hiyo kufikiria ndipo alipopata wazo ambalo aliona
lingeweza kutatua tatizo hilo.
Aliamua kumpigia simu dada yake na kumtambulisha Vicky kwake
aliamini kwa kufanya hivyo angeweza kumfanya aamini kwamba kweli anampenda kwa
dhati.
Ajawahi hata siku moja kumweleza dada yake habari za mapenzi
lakini siku hiyo ilimbidi ilikudhibitisha penzi la dhati alilokuwa nalo kwa
Vicky. Alipiga simu
“Hallow Dada , vipi huko wazima!”.
Aliongea Robert muda mfupi baada ya simu kupokelewa
“Safi tu mdogo wangu ,vipi wewe mzima!?”
ilsikika sauti ya upande wa pili
“Mi mzima tu Dada!”
“Unaendeleaje na masomo?”
“Salama tu Mungu anasaidia,Baba na mama wazima?”
“Wazima tu yani hakuna tatizo kabisa”.
“Dada nina habari mpya”.
“Zipi hizo!?”
“Kuhusu mimi”
“Nini?”.
“Nina mpenzi sasa!”.
“Mpenzi!!!”
“ndio Dada anaitwa Vicky tunapendana sana!”
“Hongera zako”
“Asante, yupo hapa nataka uongee nae”
“mpe simu basi niongee nae wifi yangu”
“haya huyu hapa”
“Shikamoo”
Vicky alisalimia
“Malhaba Vicky hujambo!”
“Sijambo!”
Vicky aliitikia
“Nimefurahi kuku fahamu Vicky , niambie kweli unampenda
mdogo wangu?”
Rehema dada yake Robert aliuliza swali hilo
na kutega sikio lake kwa makini iliasikie jibu atakalopewa
na Vicky
“Ndio dada nampenda sana”
Vicky aliitikia haraka haraka
“Kweli?”
Aliuliza tena
“Kabisa” aliitikia
“Nimefurahi kusikia hivyo, ila naomba uniahidi kitu kimoja”
“kitu gani?”
“Niahidi kwamba hautamuumiza mdogo wangu”
“Nakuahidi”
“ahsante sana”
“Na wewe pia”
“Haya mpe simu Robert”
“Sawa kwaheri”
“Hallow dada”
“Robert japo sijamuona lakini nahisi Vicky ni msichana mzuri
hongera kwa kuchagua”
“Asante dada!”
“Okey bye!” ( sawa kwa heri! )
“Bye!” ( kwa heri )
Robert aliitikia na kisha kukata simu, moyo wake ulikuwa
umejaa furaha tupu,
alifurahishwa sana na kitendo cha Rehema kumfurahia Vicky na
pia alifurahia kitendo cha kufanikisha lengo lake la kumsibitishia Vicky kwamba
kweli anampenda kwa dhati.
“Umeamini vicky umeamini kwamba kweli nakupenda eh!”
“Robert mimi nakuamini , nakuamini kwa asilimia zote naomba
usiwe na wasiwasi kabisa”
“Kweli Vicky!”
“Kabisa”
Vicky aliongea na kisha kumsogelea Robert
“Mwaa!”
alimbusu Robert shavuni, busu hilo lilifika mpaka moyoni kwa
Robert na kumfanya azidi kupagawa na penzi hilo na kujiona yupo katika dunia ya
peke yake , yeye naVicky tu kama ambavyo Adam na Eva walivyokuwa katika bustani
ya Edeni.
Vicky alizidi kufurahi pale alipoona Robert anazidi
kuchanganyikiwa na penzi. Akiamini kwamba hali hiyo ingemfanya awe na uwanja
mpana wa kupata pesa toka Robert ambae alikuwa tayari kuongea kila aina ya
uongo kwa wazazi wake ili waweze kumtumia pesa zaidi ili aweze kumpatia Vicky.
Vicky aliwasimulia rafiki zake juu ya hatua ya Robert
kumtambulisha kwa dada yake
“Nikamwamkia akaitikia ,akasema nimefurahi kukufahamu
,akaniuliza kama kweli nampenda mdogo wake nikamjibu ndio na tena akaniomba
nimuahidi kwamba sito muumiza mdogo wake pia nikamuahidi”
Vicky alimaliza kuongea kauli hiyo na kuanza kucheka ambapo
suzy nae akaanza kucheka pia.
“Umempatia kweli,saizi utakuwa unachuna kotekote”
Suzy aliongea na kisha kuendeleza kicheko pamoja na Vicky.
Tatizo lilikuwa kwa Anita ambae tangu walipoanza mazungumzo
hayo mpaka muda huo yeye alikuwa amebaki kimya tu .kitendo hicho kiliwafanya
Vicky na Suzy wabaki wakimshangaa kwani hiyo haikuwa kawaida yake.
“Vipi Anita mbona hivyo!?”.
Aliuliza Vicky kwa mshangao
“Siwezi kuendelea kuunga mkono huo ubaya wako”
“Ubaya gani !?” ,
Vicky aliuliza huku bado akiwa katika hali ya kushangaa
,hakuelewa kabisa kitu ambacho Anita anakizungumzia.
“Ukatili huo unao mfanyia mtoto wa watu!”
aliongea Anita kwa ukali
“Ukatili!!”.
“Ndio ukatili, huwezi kumchezea mtoto wa watu kiasi hicho”.
“Mbona sikuelewi Anita!?”
“Unielewi nini unavyomuongopea Robert unafikiri huo sio
ukatili eeh, amekukosea nini mtoto watu mpaka umfanyie yote hayo!?”.
Anita aliongea kwa ukali huku Vicky na Suzy wakiwa midomo
wazi kwa mshangao hawakutegemea kabisa kwamba Anita angediriki kuongea maneno
kama hayo mbele yao.
Ilikuwa ni ajabu kweli kwao kwani Anita ni rafiki yao lakini
sasa ameonyesha moyo wa usaliti
“anita kama mimi namuongopea Robert wewe inakuhusu nini?”
aliuliza Vicky kwa ukali
“Hata kama hainihusu lazima nikwambie ukweli umezidi Vicky”
Anita alijibu kwa kufoka, Vicky alifoka na Anita alifoka pia
yani hakukuwa na maelewano kabisa.
“Kama mimi nimezidi sasa wewe sasa inakuhusu nini?”
“Hapana Vick….”
Suzy alimkatisha
“Hapana nini Anita wewe hayo haya kuhusu ni mambo ya Robert
na Vicky we unaongea kama nani?”
Suzy nae alifoka
“Suzy na wewe unamuunga mkono!?”
aliuliza Anita kwa mshangao, alimshangaa Suzy sababu yeye
ndio alikuwa mtu wa kwanza kumteta Vicky karibu kila siku Vicky alipokuwa mbali
nao akidai Vicky anafanya vibaya huku akilaani kitendo hicho lakini ajabu
katika kumweleza Vicky ukweli anaamua kugeuka kama kinyonga na kujifanya yuko
upande wa Vicky
“Sasa kumbe ulifikiri mimi ni msariti kama wewe, unajifanya
rafiki kumbe una lako moyoni mnafiki mkubwa we!”
aliongea Suzy kwa nyodo.
“Na kwa taarifa yako hatuiitaji kampani yako tena na
ukijifanya unaleta kidomodomo chako tuta kufunza adabu!”
Vicky aliongea kauli hiyo kwa ukali akijaribu kumtisha Anita
, sababu alihisi kwamba Anita anaweza kumweleza Robert ukweli. Jambo Vicky hakutaka litokee kabisa kwani
lingemfanya akose hela ambazo alikuwa
anazipata kwa kumchuna Robert. Anita alitishika na maneno ya Vicky sababu
alilijua balaa lake akitibuliwa,ujasiri wote aliokuwa nao ulimwisha akabaki
kimya kwa nukta kadhaa huku uso wake ukionyesha wazi wasiwasi aliokuwano.
Lakini hata hivyo hakutaka kuishia hapo moyo wake ulimsukuma
kuongea zaidi
“Poa tu hata mkinitenga ,lakini mambo hayo lazima yawatokee
puani”.
Aliongea Anita kwa wasiwasi huku akirudi nyuma ambapo
aligeuka nyuma kuanza kuondoka haraka aliogopa kupigwa kwani alijua Vicky ana uwezo
huo .
“Eti yatatutokea puani mjinga kweli huyu!”
aliongea Vicky huku akimcheka Anita ,walicheka pamoja na Suzy huku
wakigonganisha mikono yao hawakujali tena urafiki wao na anita , sababu anita
alishawaasi na kuwasaliti.
***
MWISHO WA KITABU CHA KWANZA
Инстраграмм являться самой популярной на данный момент площадкой для продвижения своего бизнеса. Но, как показывает практика, люди гораздо чаще подписываются на профили в каких уже достаточное количество подписчиков. В случае если заниматься продвижение своими силами, потратить на это можно очень немало времени, потому гораздо лучше обратиться к спецам из Krutiminst.ru подробнее https://fxprimer.ru/index.php?topic=18008.14745
ReplyDelete